KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

Tenga ni kusuka au kunyoa leo


UCHAGUZI mkuu wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) umepangwa kufanyika leo kwenye hoteli ya JB Belmont mjini Dar es Salaam.
Katika uchaguzi huo, mwenyekiti wa sasa wa CECAFA, Leodegar Tenga atakuwa akitetea nafasi hiyo dhidi ya Fadoul Hussein wa Djibouti.
Kwa sasa, Fadoul ni makamu mwenyekiti wa baraza hilo, lakini ameamua kuwania wadhifa wa juu kwa kumpinga bosi wake.
Uamuzi wa Fadoul kugombea nafasi hiyo, unamweka Tenga kwenye wakati mgumu kwa vile atalazimika kutegemea zaidi kura za nchi jirani ya Tanzania.
Kutokana na mazingira yalivyo, Fadoul atategemea zaidi kura kutoka Djibouti, Eritrea, Somalia na Sudan wakati kura za Tenga huenda zikatoka katika nchi za Tanzania Bara, Zanzibar, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Hata hivyo, Tenga ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kushinda wadhifa huo kutokana na kuungwa na nchi nyingi zilizo wanachama wa baraza hilo, akiwemo Katibu Mkuu, Nicholas Musonye.
Uchunguzi wa Burudani umebaini kuwa, nchi nyingi zinamuunga mkono Tenga kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi, uwazi na pia ushirikiano na viongozi wenzake.
Tenga ndiye aliyeiwezesha CECAFA kupata udhamini wa michuano ya Kombe la Chalenji kutoka Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kwa miaka miwili mfululizo na kuhudhuriwa na mashabiki wengi zaidi kuliko nchi zingine.
Musonye alikaririwa hivi karibuni akisema kuwa, baraza lake linafurahia zaidi michuano hiyo kufanyika hapa nchini kutokana na kuwepo kwa udhamini mzuri na pia idadi kubwa ya mashabiki wanaofika uwanjani.
Mbali na uchaguzi wa mwenyekiti, pia watachaguliwa wajumbe wanne wa kamati ya utendaji. Wanaogombea nafasi hizo ni wajumbe wanane.
Wagombea hao ni Abdiqani Saeed Arab (Somalia), Tariq Atta Salih (Sudan), Justus Mugisha (Uganda), Tesfaye Gebreyesus (Eritrea), Hafidh Ali Tahir (Zanzibar), Sahilu Wolde (Ethiopia), Raoul Gisanura (Rwanda) na Abubakar Nkejimana (Burundi).

1 comment: