KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 30, 2011

Hatimaye Aki afunga ndoa


LAGOS, Nigeria
HATIMAYE msanii nyota wa filamu wa Nigeria, Chinedu Ikedieze amefunga ndoa na mchumba wake wa muda mrefu, Nneoma Hope Nwajah.
Harusi hiyo ya kimila ilifanyika Jumamosi iliyopita kwenye kanisa katoliki la St. Theresa lililopo Obolo, Isiala Mbano, Jimbo la Imo.
Miongoni mwa watu maarufu waliohudhuria harusi hiyo ni pamoja na wacheza filamu nyota nchini humo, Segun Arinze, Uche Jombo, Oby Edozien na Ejike Asiegbu.
Watu wengine maarufu waliohudhuria harusi hiyo ni Gavana wa jimbo la Abia na mkewe pamoja na swahiba mkubwa wa Aki, Osita Iheme ‘Ukwa’.
Katika harusi hiyo, Aki alikuwa kivutio kikubwa kwa wageni waalikwa kutokana na kuvaa kofia na miwani myeusi pamoja na kushika fimbo kubwa ya kutembelea.
Maharusi hao wawili walioanza kuchumbiana miaka mitatu iliyopita, walitunzwa fedha nyingi na wageni waalikwa na muda wote walionekana kujawa na furaha kubwa.
Sherehe nyingine ya harusi hiyo imepangwa kufanyika Desemba 10 mwaka huu mjini Lagos.

1 comment: