KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

Mr. Ibu, mkewe wapata mtoto


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu mwenye vituko nchini Nigeria, John Okafor amefanikiwa kupata mtoto wa kike baada ya mkewe kujifungua.
Okafor, maarufu zaidi kwa jina la Mr. Ibu, amepokea taarifa hizo kwa furaha kubwa, ikiwa ni pamoja na kuandaa hafla fupi ya kumpongeza mkewe kwa kujifungia salama.
Habari kutoka kwa watu wa karibu na mcheza filamu huyo zimeeleza kuwa, mkewe, Stella Maris alijifungua siku chache zilizopita.
Kwa mujibu wa habari hizo, watu mbalimbali wamemtumia Mr. Ibu na mkewe salamu za pongezi na kuwatakia maisha mema na marefu.
Mr. Ibu ni mmoja wa wacheza filamu maarufu wa Nollywood, akiwa anavutia zaidi kuchezesha filamu za vichekesho.
Alianza kujipatia umaarufu kupitia filamu ya Mr. Ibu aliyocheza kwa kushirikiana na Osita Iheme (Aki) mwaka 2004.

No comments:

Post a Comment