KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 16, 2011

JIM IYKE MATATANI


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Jim Iyke amefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutapeli Naira milioni 15 za Nigeria.
Jim alifikishwa mahakamani mjini Abuja wiki iliyopita kwa tuhuma za kumtateli Habiba Abubakar.
Kabla ya Jim kufunguliwa kesi hiyo, Habiba aliwasilisha malalamiko kwa Kamanda wa Polisi wa Abuja, Agosti 8 mwaka huu, akimtaka kuchunguza tuhuma hizo.
Katika kesi hiyo, Jim anatuhumiwa kumtapeli Habiba kiasi hicho cha pesa, kupitia kampuni yake ya Untamed Records Ltd.
Imedaiwa kuwa, mara baada ya Jim kulipwa pesa hizo, aliziingiza kwenye akaunti yake binafsi na kufanya manunuzi ya vitu vya thamani sehemu mbalimbali duniani. Mlalamikaji alidai kuwa, kila alipokuwa akidai pesa hizo, mtuhumiwa alimtishia kumpiga na kumuua.
Jim alikanusha tuhuma hizo na kupewa dhamana ya Naira 500,000 na wadhamini wawili.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 9 mwaka huu itakapotajwa tena mahakamani.

1 comment: