KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

SMG afurahia kuitwa Kilimanjaro Stars

MSHAMBULIAJI Saidi Maulid ‘SMG’ anayecheza soka ya kulipwa nchini Angola, amesema amefurahia kuitwa kwenye kikosi cha Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars kitakachoshiriki katika michuano ya mwaka huu ya Kombe la Chalenji.
SMG alisema hayo mjini Dar es Salaam juzi, alipokuwa akizungumzia kuitwa kwake kwenye kikosi hicho baada ya kuachwa kwa zaidi ya miaka mitano.
Alisema kwa mchezaji yeyote wa kulipwa anayecheza nje ya nchi yake, huwa ni fahari kubwa kwake kuitwa kwenye timu ya taifa kwa sababu kunaonyesha anavyothaminiwa.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu za Simba na Yanga alisema, amekuwa akiisubiri nafasi hiyo kwa muda mrefu na baada ya kuipata amepania kuonyesha uwezo wake.
Hata hivyo, SMG alisema kufanya vizuri kwa Kilimanjaro Stars katika michuano hiyo kutategemea ushirikiano wa wachezaji uwanjani na kutiwa moyo na mashabiki.
Alisema wao kama wachezaji, watajitahidi kucheza kadri ya uwezo wao, lakini wanahitaji sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki.
SMG aliichezea Taifa Stars mwanzoni mwa miaka ya 2000 ilipokuwa chini ya makocha wazalendo na baadaye Marcio Maximo kutoka Brazil, lakini alitemwa baada ya kwenda Angola.
Awali, SMG hakuwemo kwenye kikosi hicho, lakini makocha Charles Boniface Mkwasa na Jamhuri Kihwelu walilazimika kumwita baada ya kuumia kwa John Bocco.
Mkataba wa mshambuliaji huyo kucheza Angola unatarajiwa kumalizika Desemba 2012.

No comments:

Post a Comment