KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, November 23, 2011

AKI: Nampenda sana mchumba wangu




Asimulia walivyokutana, kupendana na kuamua wafunge ndoa
LAGOS, Nigeria
HATIMAYE mcheza filamu machachari wa Nigeria, Chinedu Ikedieze ameelezea jinsi alivyokutana na mchumba wake, Nneoma Hope Nwajah na kufikia uamuzi wa kufunga ndoa.
Chinedu, maarufu kwa jina la Aki na Nneoma, wanatarajia kufunga ndoa ya kimila keshokutwa katika kanisa Katoliki la St Theresa lililopo Obolo, Isiala Mbano katika jimbo la Imo.
Aki alisema mjini hapa wiki iliyopita kuwa, alianza kuwa na uhusiano na binti huyo miaka mitatu iliyopita baada ya kukutana naye mjini Lagos.
“Nilikutana naye Lagos na mara moja tukajikuta tukipendana. Ndiye pekee ninayempenda katika maisha yangu. Hakuna kingine kinachoweza kututenganisha zaidi ya kifo,”alisema msanii huyo. Aki, ambaye alianza kujipatia umaarufu mwaka 2003, alipocheza filamu ya Aki na Ukwa, akishirikiana na rafiki yake Osita Iheme, alisema mchumba wake huyo ni mweledi wa mambo mengi.
Alipoulizwa mchumba wake huyo alisema nini kuhusu kile anachovutiwa nacho kwake, Aki alisema: “Alisema nimekuwa mtu mzima, mwelewa, mwenye busara na upendo.”
Je, ni watoto wangapi, ambao Aki angependa kuzaa na mkewe?
“Hawatazidi watatu bila kujali jinsia zao,”alisema Aki, ambaye amecheza filamu nyingi zaidi kwa kushiriki na Osita.
Aki alisema pia kuwa, anampenda mkewe mtarajiwa kwa sababu ya umbo lake zuri alilopewa na Mungu.
Kwa sasa, Nneoma anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 20, sura yake ni jalili na ni mcha Mungu wa ukweli.
Imeelezwa kuwa, ‘bestiman’ wa Aki katika ndoa hiyo atakuwa swahiba wake, Osita.
Aki anaamini uamuzi wake wa kufunga ndoa na Nneoma utamwingiza katika ulimwengu mpya kwa vile mwonekane wake utakuwa tofauti na wa sasa.
Kabla ya kukutana na Nneoma, Aki alimchumbia mwanadada Nkechi kutoka Jimbo la Delta, ambaye ni mfanyakazi wa benki, lakini hawakuweza kufunga ndoa.
Mcheza filamu huyo milionea wa Nigeria, pia aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwingine, lakini ulivunjika mapema zaidi.
Magavana watatu ni miongoni mwa watu mashuhuri walioalikwa kuhudhuria harusi ya Aki na Nneoma. Magavana hao ni Chifu T.A Orji wa Abia, Rochas Okorocha wa Imo na Peter Obi wa Anambra.
Kuna habari kuwa, sherehe za ndoa hiyo pia huenda zikahudhuriwa na Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan na mkewe.

1 comment: