KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 5, 2012

Hard Mad ahimiza uzalendo kwanza



BAADA ya ukimya wa muda mrefu, msanii machachari wa muziki wa miondoko ya dance hall na raga nchini, Hard Mad ameibuka na kibao kipya.
Hard Mad alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, kibao chake hicho kinakwenda kwa jina la Uzalendo kwanza.
Msanii huyo aliyetengeneza nywele zake kwa mtindo wa rasta alisema, kibao hicho kimelenga kukemea matendo mbalimbali yanayotokea katika jamii.
“Ninachokisisitiza katika wimbo huo ni kuwataka wafanyakazi maofisini na kwenye ofisi za serikali waweke uzalendo mbele katika kazi zao,”alisema.
Hard Mad amewataka mashabiki wake watarajie vitu vipya na vikali kwa mwaka 2012 kwa vile ameamua kutoka kivingine.
Hivi karibuni, msanii huyo aliipua kibao kikali kinachojulikana kwa jina la Ujio mpya, akiwa amemshirikisha msanii Enika.
“Napenda kuwaambia wasanii wangu kwamba watarajie vitu vya kikubwa na ujio mpya kwa sababu hata jina langu sasa limebadilika. Kwa sasa najulikana kwa jina la Mkushi Moja,”alisema msanii huyo.
Hard Mad alianza kutambulika kimuziki mwaka 2001 baada ya kutoa albamu yake ya kwanza inayojulikana kwa jina la Sina muda. Albamu hiyo ilibeba vibao vingine kadhaa kama vile ‘Ninapotaka, Malaika, Niambie na Jakia.
Albamu yake ya pili inajulikana kwa jina la Ni wewe, aliyoitoa mwaka 2006 ikiwa na vibao kama Blessing from Jah, Tamara, Give it to me’ na nyinginezo. Albamu hiyo ilipata mapokeo mazuri, ikiwa ni pamoja na kumuwezesha kutwaa tuzo ya msanii bora wa ragga/dancehall katika tuzo za muziki za Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment