KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 5, 2012

HEMED: Mademu, wake za watu sasa basi


MSANII nyota wa filamu na muziki wa kizazi kipya nchini, Hemed Suleiman amesema mademu na wake za watu kwake sasa basi.
Hemed alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, ameamua kuachana na mambo hayo kwa lengo la kuuanza mwaka 2012 kivingine.
Alisema uamuzi wake huo umelenga kuondokana na matukio yaliyomchafua na kumtia doa mwaka 2011.
“Wake za watu, mademu za watu hakuna tena 2012,”alisema msanii huyo aliyeshiriki mashindano ya Tusker Project Fame mara mbili nchini Kenya.
“Wamenifanya nigombane na watu wengi mwaka jana. Washkaji zangu wa karibu walinishusha thamani. Lazima nibadilike mwaka 2012,”alisisitiza.
Hemed alisema kwa sasa anajiandaa kupakua albamu yake, itakayokwenda kwa jina la Hedach, ambayo inatarajiwa kuingia sokoni mwezi ujao.
Mbali na kuachia albamu hiyo, amesema amepania kuingia gym kwa lengo la kupunguza unene baada ya mashabiki wake kumlalamikia kwamba amenenepa kupita kiasi.
Hemed ni miongoni mwa wasanii waliotawala vyombo vya habari mwaka jana baada ya kuandamwa na kashfa za kutembea na wake za watu pamoja na wapenzi wa marafiki zake.
Msanii huyo aliwahi kukaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akidai kuwa, fani ya filamu ndiyo iliyosababisha apapatikiwe na wanawake wengi.
Mmoja wa wasanii wa filamu wa kike, aliyeonekana kumpapatikia waziwazi Hemed ni Jennifer Raymond ‘Penina’, ambaye aliapa lazima afunge ndoa na msanii huyo.
Penina alisema hayo katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha televisheni cha Channel Five, kupitia kipindi cha Friday Night.

No comments:

Post a Comment