KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 2, 2012

AIRTEL YATOA MSAADA WA VITABU SHULE YA SEKONDARI KISAWASAWA KIROMBERO, MOROGORO

Kisawasawa Secondary School Headmaster in Morogoro, Menasi Msigwareceiving books donation from Dangio Kaniki Airtel Public relationsand Event Officer second while from left looking on is Airtel Publicrelations and Event Officer Dangio Kaniki.

Airtel Public relations and Event officer Dangio Kaniki leftchallenging one of the students in Kisawasawa Secondary School duringthe book handover ceremony held at Kisawasawa Secondary school inMorogoro, behind left is Corporate Social and Responsibility ManagerHawa Bayuni, second left is Headmaster of Kisawasawa Secondary SchoolMenasi Msigwa followed by Airtel Sales Officer Mohammed Mbamba.

Airtel Public Relations and Event Officer Dangio Kaniki (left) makinga point during the book handover ceremony in Kisawasawa SecondarySchool in Morogoro, left is the Corporate Social and ResponsibilityManager Hawa Bayuni and right is the Headmaster of Kisawasawa PrimarySchool Menasi Msigwa.


Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kwa kupitia mpango wake wa 'Airtel shule yetu' imetoa vitabu vya ziada na kiada kwa shule ya sekondari Kisawasawa ya mkoani Morogoro lengo likiwa ni kusaidiamaendeleo ya elimu mkoani hapo na kutoa huduma kwa jamii.
Hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika shule ya sekondariKisawasawa na kuhudhuriwa na wawakilishi wa shule, wanafunzi,waandishi wa habari na wafanyakazi wa Airtel ambapo vitabu vyenyethamani ya shilingi milioni mbili vilikabidhiwa kwa shule hiyo.
Akiongea wakati wa halfa ya makabidhiano ya vitabu hivyo, AfisaUhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki alisema, " Airtelinatambua kuwepo kwa uhaba wa vitabu na vifaa vya kufundishia katikashule zetu na katika kutatua changamoto hizo tunaongeza nguvu nakushirikiana na Serikali chini ya wizara ya elimu kuweza kuinua sektaya elimu.
"Tunafahamu umuhimu wa elimu katika kujikwamua na umaskini, hali ngumu ya maisha na kupata nguvu kazi ya kesho, kwa kutoa kipaumbele kwakusaidia na kuhakikisha nyenzo muhimu za kufandishia zinapatikanamashuleni ili kuweza kufikia dhamira yetu ya kusaidia jamii kwa ujumlaAirtel inatoa fulsa sawa kwa shule zote nchini na leo tumewafikiawanafunzi wa Kisawasawa Kilombero Morogoro. Tunaamini elimu ndioufunguo wa maisha hivyo tunayo malengo ya dhati kabisa katika kusaidiakuinua kiwango cha elimu.
Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule ya Sekondari ya Kisawasawa bw,Menasi Msigwa ameishukuru Airtel kwa kuwawezesha kupata vitendeakazi na kuongeza kuwa shule hiyo bado inakabiliwa na changamotonyingi katika elimu hivyo kuiomba kampuni hiyo kuendelea kuisaidiakatika mambo mengine.
Aidha alichukua fulsa hiyo kuwaasa wanafunzi kutumia na kuvitunzavitabu hivyo ili viweze kusomwa na wanafunzi wengi zaidi na kuongezakiwango cha kufaulu katika shule hiyo. Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imekuwa ikitoa misaada mbalimbali kama vile Vitabu vya shule ya sekondari, wiki iliyopita Airtel ilitoa msaada wa Vitabu kwa shule ya Mtipwa iliyopo mkoa wa Singida.
Tangu Airtel ilipoanza mpango wa kusaidia vitabu kwa shule mbali mbaliza sekondari hapa nchini, takribani miaka saba iliyopita,imeshazifikia zaidi ya shule za sekondari tofauti zipatazo 1,000nchini Hii ikiwa nikatika kurudisha faida inayoipata na kuchangiakatika huduma kwa jamii.

No comments:

Post a Comment