KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 9, 2012

WOLPER APIGA HESABU ZA MUZIKI

MCHEZA filamu machachari nchini, Jacqueline Wolper amesema anacho kipaji cha muziki, lakini bado hajaamua kujitosa kwenye fani hiyo.
Akizungumza mjini Dar es Salaam wiki hii, Jacqueline alisema wakati ukifika, huenda naye akaonyesha uwezo wake katika fani hiyo, inayoongoza kwa kuwa na mashabiki wengi nchini.
Jacqueline alisema tangu alipokuwa mdogo, aliweza kujitambua mapema kwamba anacho kipaji cha muziki, lakini hajaanza kukitumia, badala yake alijitosa kwenye filamu.
“Ukweli ni kwamba nina uwezo mkubwa sana katika fani ya muziki kuliko filamu,”alisema.
Kwa mujibu wa Jacqueline, filamu pekee, ambayo hadi sasa imemwezesha kupata malipo mazuri kuliko zingine kutokana na ushiriki wake ni Time After Time.
Alisema filamu hiyo iliyoandaliwa na Mussa Mtitu ni nzuri na ya aina yake kwa vile imeandaliwa kwa utaalam wa hali ya juu na kuhusisha matukio mengi ya mapigano.
“Napenda sana kucheza filamu za Mtitu kwa sababu ni za mapigano zaidi,”alisema.
Wakati huo huo, Jacqueline ametoa tahadhari kwa mashabiki wake kuhusu kujitokeza kwa mwanadada anayetumia jina lake kuomba fedha kwa watu mbali mbali.
Jacqueline amesema mwanamke huyo amekuwa akijitokeza mara kwa mara kwenye mitandao ya kijamii akijitambulisha kwa jina lake na kuomba misaada ya fedha.
“Huyu mtu ananijua vyema na kunifuatilia sana. Na wakati mwingine amekuwa akitumia jina la Jack Masawe, ambalo nilikuwa nikilitumia nilipokuwa shuleni,”alisema.
‘Nawaomba mashabiki wangu wajihadhari na mtu huyu kwa sababu ni tapeli,’ aliongeza.

No comments:

Post a Comment