KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 9, 2012

KISIGA AIBUKIA MTIBWA SUGAR




KIUNGO wa zamani wa klabu ya Simba, Shaaban Kisiga amesajiliwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa ajili ya msimu ujao wa ligi kuu ya Tanzania Bara.
Mratibu wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, wameamua kumsajili Kisiga kwa lengo la kukiongezea nguvu kikosi cha timu hiyo.
Bayser alisema Kisiga ameshaanza mazoezi na timu hiyo na anatarajiwa kuanza kuichezea katika michuano ya BancABC Super 8 inayoendelea kutimua vumbi kwenye viwanja mbali mbali.
Mratibu huyo alikiri kuwa, kikosi chake kitapata upinzani mkali msimu ujao kutokana na timu nyingi kufanya maandalizi mazuri na kusajili wachezaji wengi nyota.
"Ni kweli kwamba tuna kazi ngumu na nzito msimu ujao kwa vile timu nyingi zimepania kuchukua ubingwa na sisi vivyo hivyo, kwa maana hiyo tutalazimika kupambana kufa na kupona,’ alisema.
Mbali na Kisiga, Mtibwa Sugar imemrejesha kipa wake wa zamani, Shabani Kado, ambaye msimu uliopita aliichezea Yanga na Machaku Salum, aliyekuwa akiichezea Simba.
Kwa sasa, Mtibwa Sugar inafundishwa na Kocha Mecky Maxime baada ya kutimuliwa kwa kocha wa zamani, Tom Olaba kutoka Kenya.

No comments:

Post a Comment