KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, March 15, 2014

SIWEZI KUACHA UIGIZAJI ILI NIOLEWE-ANITA


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu mwenye vituko nchini Nigeria, Anita Joseph, ameamua kuachana na mumewe mtarajiwa, baada ya kumtaka aachane na kazi ya uigizaji.

Anita na mchumba wake huyo, walitarajia kufunga ndoa hivi karibuni, lakini masharti ya mwanaume huyo yalimfanya mwanadada huyo aione ndoa kuwa chungu.

Kuvunjika kwa uchumba wa wapenzi hao, kumezua maswali mengi kuhusu sababu ya kutengana kwao na Anita ameamua kuweka wazi ukweli wa mambo ili kusafisha hali ya hewa.

"Nilikataa ombi lake la kutaka kufunga ndoa na mimi kwa sababu siwezi kuwa mwanamke wa kukaa ndani. Alitaka niache kazi ya uigizaji na kuwa mwanamke wa ndani muda wote,"alisema Anina.

"Mimi si mwanamke wa aina hiyo wa kukaa nyumbani siku nzima. Napenda kufanyakazi. Napenda kuwa bize muda wote,"alisisitiza.

Anita alisema alianza kufahamiana na kijana huyo miaka miwili iliyopita kabla ya kuanzisha naye uhusiano wa kimapenzi uliodumu kwa mwaka mmoja.

"Sitaki kumtambulisha majina yake. Ninachoweza kusema ni kwamba, jina lake ni M. Ni kijana mzuri, lakini anaweza kukudhuru anapopatwa na wivu. Ananielewa nilivyo,"alisema Anita.

Kwa mujibu wa Anita, kijana huyo aliwahi kumuona kwenye televisheni kabla ya kukutana naye na tangu wakati huo, alianza kufuatilia filamu zake.

"Hataki kuniunga mkono katika kazi yangu.Anataka niachane na kazi hiyo baada ya kufunga naye ndoa,"alisema Anita.

"Hataki nitoke nje. Hapendi nijihusishe na filamu za mapenzi. Hataki watu wanitazame na mimi nionekane kwenye filamu za mapenzi. Ninalo wazo la kuolewa, lakini sina haraka ya kufanya hivyo," alisisitiza nyota huyo.

No comments:

Post a Comment