KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 20, 2014

AKI SASA AITWA BABA, AZUA GUMZO KWA KUVAA KIKE






LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Chinedu Ikedieze 'Aki', hivi karibuni aliamua kuweka hadharani picha za binti yake kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii.

Picha hizo zinamwonyesha Aki akiwa amempakata binti yake huyo mwenye umri wa miezi kadhaa, ikiwa ni miaka miwili baada ya kufunga ndoa na Nneoma.

Aki ameamua kuweka picha hizo hadharani kwa lengo la kuwafahamisha mashabiki wake kwamba, tayari anaitwa baba.

Mashabiki wengi wa filamu za Kinigeria walioziona picha hizo, wamempongeza Aki kwa uamuzi wake wa kuoa na hatimaye kuitwa baba.

Hivi karibuni, Aki na msanii mwenzake nyota wa fani hiyo, Osita Iheme 'Ukwa' walitawala vyombo vya habari baada ya kuibuka na filamu mpya inayokwenda kwa jina la The Return of Aki na PawPaw Sisters'.

Katika filamu hiyo, Aki na Ukwa wameigiza kama mabinti mapacha wanaoishi kijijini na kumpa usumbufu mkubwa baba yao kama ilivyokuwa katika filamu ya Aki na Ukwa.

Hata hivyo, filamu hiyo imezua gumzo mkubwa, huku baadhi ya mashabiki wakiipinga na wengine kuiunga mkono.

Baadhi ya mashabiki wanaoipinga wamesema, haikuwa sahihi kwa wacheza filamu hao kuigiza kama mabinti kwa kuvaa nguo za kike wakati wao ni vijana wa kiume.

Mtayarishaji wa filamu hiyo, Martin Onyemaobi na muongozaji wake, Amayo Uzo Philips, waliamua kubuni kisa kingine kinachofanana na kile cha kwenye filamu ya Aki na Ukwa, lakini kwa kuwatumia waigizaji wa kike.

Ukwa, alizaliwa Desemba 12, 1977 katika mji wa Bende ulioko kwenye Jimbo la Abia nchini Nigeria. Amejipatia umaarufu mkubwa kutokana na kucheza filamu nyingi akishirikiana na Ukwa.

Mcheza filamu huyo mwenye shahada ya mawasiliano ya umma, ameshinda tuzo nyingi, zikiwemo za mwigizaji bora wa Afrika.

Alianza kupata umaarufu kwa kucheza filamu ya Evil Men kabla ya kuibuka tena kwenye filamu ya The Last Burial. Baada ya hapo, alicheza filamu nyingi kwa kushirikiana na Ukwa, ambaye kwa sasa ndiye swahiba wake mkubwa.

1 comment: