KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, May 18, 2011

Kado atuliza mzuka Mtibwa


KIPA namba moja wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Shaaban Kado amesema, kwa sasa hana mpango wowote wa kuondoka katika timu hiyo.
Kado alisema kwa njia ya simu jana kutoka Morogoro kuwa, iwapo ataondoka Mtibwa Sugar, lengo lake litakuwa ni kwenda nje kucheza soka ya kulipwa.
Kipa huyo, ambaye pia yumo kwenye kikosi cha timu ya taifa ya vijana wa chini ya miaka 23, alisema amefikia uamuzi huo baada ya kupewa ushauri na watu mbalimbali.
Kabla ya kufikia uamuzi, Kado alisema alikuwa amepata ofa za kujiunga na klabu za Simba na Yanga kwa ajili ya msimu ujao wa ligi na michuano ya kimataifa.
"Nilipata ofa kibao, lakini nimepata ushauri wa kina kutoka kwa watu mbalimbali wanaonitakia mema, hivyo nimeamua kuendelea kuwepo ndani ya kikosi cha Mtibwa, ambako nina hakika ya ajira,"alisema mlinda mlango huyo.
Hata hivyo, Kado alisema bado anaendelea kufanya mawasiliano na baadhi ya mawakala wa wachezaji ili aweze kwenda kufanya majaribio nje ya nchi.
Aliongeza kuwa, lengo lake kubwa ni kwenda kucheza soka ya kulipwa nje ya Tanzania kwa lengo la kuinua zaidi kipaji chake na pia kuongeza mapato.

No comments:

Post a Comment