KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 23, 2014

ALICHI: SIWEZI KUCHEZA FILAMU ZA NGONO


LAGOS, Nigeria
CHIZZY Alichi ni mwigizaji mpya wa filamu nchini Nigeria, lakini ameweza kujipatia sifa na umaarufu kutokana na staili yake ya uigizaji.

Ni mwigizaji mwenye umbo lenye mvuto, akiwa na macho ya kuvutia. Sifa zake katika kucheza filamu, hazina tofauti na zile za Genevieve Nnaji, Ini Edo au Mercy Johnson.

Akihojiwa na mtandao wa naijerules hivi karibuni, Alichi alisema ana uwezo mkubwa wa kucheza nafasi yoyote atakayopangiwa na mtayarishaji wa filamu.

Alichi anasema mwanaume wa kwanza kupigana naye mabusu kwenye filamu, alikuwa Kenneth Okonkwo. Anasema alijisikia raha kufanya hivyo kutokana na ukweli kwamba, siku zote amekuwa akivutiwa na uigizaji wa Okonkwo.

"Nimepigana mabusu mara nyingi na waigizaji tofauti. Mara ya kwanza ilikuwa kwa Okonkwo,"amesema Alichi. 

"Ni mwigizaji ninayevutiwa naye, hivyo kupigana naye mabusu kilikuwa kitendo chenye maana kubwa kwangu. Aliyapokea vizuri mabusu yangu," aliongeza binti huyo mantashau.

Alichi amesema si kweli kwamba, msanii wa filamu anaweza kupata umaarufu kwa kucheza filamu ya ngono. Amesema binafsi anaweza kucheza nafasi yoyote katika filamu, lakini siyo ile itakayomwonyesha akiwa uchi.

"Nataka niwe mfano mzuri wa kuigwa na wasanii wengine, na pia natarajia kuolewa na kupata watoto. Watajisikiaje kumuona mama yao akicheza filamu ya aina hiyo?" Amehoji.

"Wazazi wangu wananiunga mkono, lakini hawawezi kufanya hivyo iwapo nitacheza filamu za ngono. Naweza kuvaa mavazi yenye mvuto wakati wa kucheza filamu, lakini sio kuwa uchi ama kucheza filamu ya ngono," amesisitiza.

Alichi amesema kwa sasa haoni aibu anapokuwa mbele ya kamera kama ilivyokuwa zamani kwa vile ameshaizoea kazi hiyo. Anasema anapenda uigizaji na amekuwa akiifanyakazi hiyo kwa umakini mkubwa.

Hata hivyo, Alichi amesema linapokuja suala la maisha yake binafsi, bado yeye ni msichana mwenye aibu.

No comments:

Post a Comment