KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 20, 2011

Asamoah kuuzwa kwa mkopo Moro United


KAMATI ya Usajili ya klabu ya Yanga imeanza mchakati wa kuongeza nguvu kwenye kikosi cha timu hiyo ikiwa ni pamoja na kuwauza baadhi ya wachezaji wake.
Habari zilizopatikana jana kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa, kwa kuanzia, kamati hiyo imeamua kumuuza kwa mkopo mshambuliaji wake, Kenneth Asamoah kwa klabu ya Moro United.
Kwa mujibu wa habari hizo, Asamoah huenda akauzwa kwa Moro United wakati wa usajili wa dirisha dogo unaotarajiwa kufanyika Januari mwakani.
Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo alilieleza gazeti la Burudani kuwa, uamuzi wa kumuuza Asamoah umefikiwa kutokana na kiwango chake kushuka.
Mjumbe huyo alisema, kamati yake imekuwa ikiandaa ripoti ya kila mchezaji ili iwe rahisi kujua uwezo wao na nafasi yao kwa Yanga.
“Lengo letu ni kujenga timu imara kwa ajili ya michuano ya klabu bingwa Afrika mwakani,”alisema mjumbe huyo, ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini.
Hatua hiyo ya Yanga imekuja siku chache baada ya mfadhili wa zamani wa klabu hiyo, Yussuf Manji kuushutumu uongozi kwa kusajili wachezaji wengi wasiokuwa na uwezo, wakiwemo kutoka nje ya nchi.
Wachezaji wengine, ambao wapo njia panda kuuzwa na klabu hiyo ni pamoja na Pius Kisambale na Godfrey Bonny.

No comments:

Post a Comment