KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 22, 2011

Kipre Tchetche nje wiki mbili

MSHAMBULIAJI Kipre Tchetche wa Azam ametakiwa kupumzika kucheza soka kwa muda wa wiki mbili kufuatia kuumia mguu hivi karibuni.
Mratibu wa Azam, Nassor Idrisa alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Tchetche anasumbuliwa na maumivu ya misuli.
Nassor alisema tayari mchezaji huyo kutoka Ivory Coasta ameshafanyiwa uchunguzi wa tatizo hilo na kuanza kupatiwa matibabu.
Alisema kutocheza kwa mchezaji huyo katika mechi kati ya Azam na Yanga kulitokana na maumivu hayo na si vinginevyo.
Akizungumzia mwenendo wa ligi ulivyo hivi sasa, Nassor alikiri kuwa, ligi ya msimu huu ni ngumu kwa vile kila timu imepania kushinda.
Wakati huo huo, uongozi wa klabu ya Simba umesema, beki Amir Maftah anatarajiwa kufanyiwa uchunguzi wa kina katika kifundo chake cha mguu.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange 'Kaburu' alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Maftah aliumia mguu mwishoni mwa wiki iliyopita wakati timu hiyo ilipomenyana na Kagera Sugar mjini Bukoba.
Kaburu alisema tayari mchezaji huyo ameshaanza kupatiwa matibabu, lakini atafanyiwa uchunguzi wa kina ili kubaini ukubwa wa tatizo hilo.

No comments:

Post a Comment