KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 9, 2014

MUJUNI KUZIHUKUMU SIMBA NA YANGA OKTOBA 18




MWAMUZI Israel Mujuni Nkongo anatarajiwa kuchezesha pambano la watani wa jadi la ligi kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Yanga.


Pambano hilo litachezwa Oktoba 18 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mtendaji mkuu wa Bodi ya Ligi Tanzania, Silas Mwakibinga alisema waamuzi wa pembeni watakuwa ni Fednandi Chacha kutoka Mwanza na John Kanyenye kutoka Mbeya.

Alisema Mwamuzi wa mezani atakuwa ni Hashimu Abdalah na Kamishna wa mechi hiyo ni Salum Kikwamba.

Alisema maandalizi ya mechi hiyo yanaendelea vema huku timu zote zikiwa katika maandalizi kwa ajili ya mchezo huo.

Tayari Simba wamekwea pipa juzi kuelekea Afrika Kusini kujiandaa na mchezo huo huku Yanga ikiendelea kujifua katika viwanja vya Loyola Dar es Salaam.

Mwakibinga alisema mbali na mechi hiyo pia kwa upande wa timu nyingine mechi zitaendelea kama kawaida ambapo Mtibwa Sugar itacheza dhidi ya Polisi Morogoro katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Pia Ndanda FC itashuka dhidi ya Ruvu Shooting katika uwanja wa Nangwanda mjini Mtwara, Kagera Sugar dhidi ya Stand United utakaochezwa uwanja wa Kaitaba na Coastal Union dhidi ya Mgambo JKT katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Alisema pia siku hiyo kutakuwa na mechi kati ya Azam na Mbeya City utakaochezwa uwanja wa Sokoine jijini Mbeya na Tanzania Prison itaumana dhidi ya JKT Ruvu katika uwanja wa Azam Complex Chamazi Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment