KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, March 7, 2012

Segun Arinze apata mtoto wa pili

LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu mwenye umbile la miraba minne nchini Nigeria, Segun Arinze amepata mtoto wa pili.
Habari zilizoufikia mtandao wa nigeriafilms wiki hii umeeleza kuwa, mke wa Arinze, Julie alijifungua mtoto wa kike Machi 2 mwaka huu mjini Texas, Marekani.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, Julie alijifungua mtoto huyo saa tisa na nusu usiku.
Habari hizo zimeeleza kuwa, hali ya Julie na mtoto huyo inaendelea vizuri.
Juhudi za kumtafuta Arinze ili athibitishe habari hizo hazikuweza kufanikiwa kwa vile hakuwa akipokea simu yake ya mkononi.
Arinze ni rais wa chama cha waigizaji nchini Nigeria (AGN) na anatarajiwa kumaliza muda wake hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment