KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 22, 2012

Martha Mlata, Kilahiro kuitoa 'Tulia miguuni mwa Yesu'

MBUNGE wa Viti Maalumu mkoa wa Singida, Martha Mlata, anatarajiwa kusindikiza uzinduzi wa albamu ya ‘Tulia miguuni kwa Yesu.
Martha, ambaye anatamba na nyimbo mbalimbali za injili, ataungana na wasanii wengine akiwemo Upendo Kilahiro kuitoa albamu hiyo ya nyota mwenzao Stella Joel.
Uzinduzi wa ‘Tulia miguuni mwa yesu’ unatarajiwa kufanyika Machi 25, mwaka huu, katika Ushirika wa KKKT Mabibo External.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, jana, Stella alisema albamu hiyo inasubiri kwa hamu kubwa na mashabiki wa muziki wa injili nchini.
Alisema mbali na Martha na Upendo, wasanii mbalimbali wa injili watashiriki kwenye uzinduzi wa albamu hiyo.
Stela aliwataja baadhi ya wasanii kuwa ni Addo November, John Shabani, Debora Saidi, Janeth Mrema, Victor Aron na Kwaya ya Joy Bringers.
Stella alisema maandalizi yote kwa ajili ya uzinduzi huo yamekamilika na kwamba, bado anaendelea na mazoezi makali ili kukonga nyoyo za mashabiki wake.
“Maandalizi yote yamekamilika na wasanii wanaendelea na mazoezi makali kwa ajili ya kukonga nyoyo za mashabiki wetu. Tulia miguuni kwa yesu ni albamu yenye ujumbe na mafundisho mengi, hivyo Mungu atuongoze salama wakati ufike,” alisema.
Stella alisema katika uzinduzi huo, mgeni rasmi atakuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Massaburi, ambaye ataongoza mamia kushuhudia uzinduzi huo na kwamba, hakutakuwa ni kiingilio.

No comments:

Post a Comment