KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, September 1, 2016

YONDANI AMCHEFUA MKWASA, SAMATTA KUUNGANA NA STARS IFIKAPO NIGERIA



KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Charles Boniface, ameelezea kuchukizwa kwake na kitendo cha beki Kevin Yondani wa Yanga kushindwa kuripoti kwenye kambi ya timu hiyo.

Yondani amegoma kuripoti kwenye kambi ya Taifa Stars,inayojiandaa kwa mchezo wake wa michuano ya Afrika dhidi ya Nigeria.

Akizungumza na waandishi  wa habari jana, Boniface alisema ameshangazwa na ukimya wa Yondani, ambaye hajatoa taarifa yoyote kuhusu kushindwa kwake kuripoti kambini.

Boniface alisema amejaribu kumpigia simu Yondani kwa siku mbili,lakini hakufanikiwa kumpata.

Taifa Stars iliondoka nchini jana usiku kwenda Nigeria, ambako itacheza na timu ya taifa ya nchi hiyo Jumamosi.

Mechi hiyo itakuwa ya kukamilisha ratiba kwa Taifa Stars kwa vile imeshatolewa.

Wakati huo huo, mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayechezea timu ya Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta anatarajiwa kuungana na timu hiyo nchini Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017).

Hadi mchana wa leo Agosti  29, 2016 ni Kelvin Yondan pekee kutoka Young Africans ambaye hakuripoti kwenye kikosi hicho kilichopiga kambi yake kwenye Hoteli ya Urban Rose iliyoko katikati ya jiji la Dar es Salaam. Kipa mpya wa timu hiyo, Said Kipao alijiunga na timu hiyo mara moja baada ya kuteuliwa na Kocha Mkuu, Charles Boniface Mkwasa.

Taifa Stars inatarajiwa kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo huo dhidi ya timu ya taifa ya nchi hiyo, Super Eagles utakaofanyika Septemba 3, 2016. Licha ya mchezo huo kuwa sehemu ya mchuano wa kuwania nafasi ya kucheza fainali hizo za AFCON 2017 huko Gabon, lakini utakuwa ni wa kukamilisha ratiba baada ya Misri kufuzu kutoka kundi G ambalo mbali ya Nigeria na Tanzania, pia ilikuwako Chad ambayo iliyojitoa katikati ya mashindano.

No comments:

Post a Comment