KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, February 28, 2014

GENEVIEVE, MIKEL OBI WATANUA 'SAUZI'





LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI nyota na mwenye mvuto nchini Nigeria, Genevieve Nnaji hivi karibuni alionekana nchini Afrika Kusini akivinjari na mwanasoka nyota wa klabu ya Chelsea na timu ya Taifa ya Nigeria, Mikel Obi.

Genevieve na Obi walionekana wakiwa pamoja kwenye uwanja mmoja wa ndege nchini humo kabla ya kukwea pipa dogo la kukodi kwenda kusikojulikana.

Mwanadada huyo mwenye mtoto mmoja, alikuwa wa kwanza kuwasili kwenye uwanja huo kwa gari dogo la kifahari kabla ya Obi naye kuwasili akiwa kwenye gari lingine la kifahari lenye rangi ya kumeremeta.

Haikuweza kufahamika mara moja nyota hao walikwenda Afrika Kusini kufanya nini na iwapo wana uhusiano wa kimapenzi.

Katika hatua nyingine, Genevieve amewataka wanawake duniani kujenga utamaduni wa kulindana kama wanavyofanya kwa mabinti zao.

Genevieve amesema hayo wiki hii kupitia akaunti yake ya twitter, kauli ambayo imedhihirisha kwamba ni mama anayewajali wanawake wenzake.

"Mtoto wa kike ataushika mkono wako kwa muda, lakini ataushika moyo wako milele. Mlinde kila mwanamke kama utakavyomlinda binti yako," ameeleza Genevieve kwenye ujumbe wake huo.

No comments:

Post a Comment