KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, December 8, 2016

SIMBA, YANGA KURUDIANA DESEMBA 18


MZUNGUKO wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara unatarajiwa kuanza Desemba 17, mwaka huu wakati mchezo wa mahasimu wa jadi, Simba na Yanga utakuja Februari 18, mwakani.
Baada ya mapumziko ya tangu Novemba 10, kufuatia kumalizika kwa mzunguko wa kwanza kitimutimu cha Ligi Kuu kinarejea Jumamosi ya Desemba 17, mabingwa watetezi, Yanga SC kufungua dimba na JKT Ruvu Stars Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Mechi nyingine siku za siku hiyo, Mbeya City watamenyana na Kagera Sugar Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, Mwadui na Toto Africans Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga na Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani.
Vinara wa ligi hiyo, Simba wataanza kampeni ya kuwania taji la kwanza baada ya miaka minne Jumapili ya Desemba 18 watakapoifuata Ndanda Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, siku ambayo Mbao FC watamenyana na Stand United Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, African Lyon na Azam Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na Prisons na Maji Maji Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

No comments:

Post a Comment