KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 17, 2016

YANGA, AZAM HAKUNA MBABE


YANGA na Azam jana zilizidi kutoa mwanya kwa Simba kujikita kileleni mwa ligi kuu, baada ya kutoka suluhu katika mechi ya ligi kuu iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kutokana na sare hiyo, Yanga sasa inazo pointi 15 baada ya kucheza mechi nane, ikitoka sare mechi tatu, imefungwa moja na kushinda nne.

Kwa upande wa Azam, sare hiyo imeifanya iwe na pointi 12 baada ya kucheza mechi tisa, ambapo imetoka sare mechitatu, imefungwa tatu na kushinda tatu.

Licha ya timu zote mbili kushambuliana kwa zamu, pambano hilo halikuwa na mvuto uliotarajiwa, kutokana na wachezaji wa timu hizo kuonyeshana ubabe zaidi.

No comments:

Post a Comment