KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, June 12, 2014

WABRAZIL KUTUMIA KAA KUTABIRI MATOKEO


Salvador, Brazili

KAMA ilivyokuwa katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010 zilizofanyika Afrika Kusini, utabiri wa kutumia wanyama katika kinyang’anyiro kinachoanza leo Brazili umeibuka tena, huku mwenyeji Brazil akiwa na matumaini na mtabiri wake-kaa.

Akitumia kubashiei kwa kuchagua chakula, kaa huyo aliyepachikwa jina la Kichwa Kikubwa, juzi alitabiri kwamba mwenyeji huyo ataibuka na ushindi dhidi ya Croatia katika mechi ya ufunguzi.

Kichwa Kikubwa ndilo jibu kwa Pweza Paulo wa Ujerumani, ambaye alianza kutumika katika michuano ya mwaka 2010 na kusababisha msisimko mkubwa duniani.

Katika zizi la kaa lililoko Praia do Forte Kaskazini mwaka Salvador, kaa huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 25 juzi alipewa kuchagua kati ya kula samaki aliyening’inizwa kwenye bendera ya Brazil na mwingine kwenye bendera ya Croatia.

Baada ya kujaribu kula samaki aliyekuwa amening’inizwa kwenye mpira ikimaanisha matokeo ya sare, Kichwa Kikubwa aliamua kuchagua anayewakilisha Brazili.

Kundi dogo la watu waliokuwa wakishuhudia hali hiyo lilishangilia kutokana na uchaguzi huo wa Kichwa Kikubwa.

Wachina wameamua kumtumia kundi la ndama wa dubu aina ya panda kutabiria timu yao katika michuano hiyo.

Hata hivyo mwaka 2010 utabiri wa Paul ulikwama baada ya Ujerumani kupoteza mechi kwa Hispania katika nusu fainali ya mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment