KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, October 13, 2012

HATMA YA UCHAGUZI DRFA J'NNE


Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekamilisha usikilizaji rufani zilizokatwa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA.

Ili kujiridhisha kuhusu uamuzi wote uliofanywa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA kuhusu waombaji uongozi wote wa DRFA waliopitishwa na ambao hawakupitishwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Kamati itatangaza uamuzi wake kuhusu mchakato mzima wa uchaguzi wa DRFA siku ya Jumanne, Oktoba 16, 2012.

Kutokana na hali hiyo, Uchaguzi wa DRFA uliokuwa ufanyike Oktoba 14, 2012 umeahirishwa hadi hapo uamuzi kuhusu uchaguzi huo utakapotangazwa Jumanne, Oktoba 16, 2012.

Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Katibu- Kamati ya Uchaguzi TFF

No comments:

Post a Comment