KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, January 15, 2013

KESHI: HAKUNA MWENYE NAMBA YA KUDUMU NIGERIA

LAGOS, Nigeria WACHEZAJI wa timu ya soka ya Taifa ya Nigeria wametahadharishwa kuwa, hakuna mchezaji mwenye namba ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

Tahadhari hiyo imetolewa na Kocha Mkuu wa Nigeria, Stephen Keshi alipozungumza na waandishi wa habari mjini hapa juzi kuhusu maandalizi ya timu hiyo kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika.

"Nataka wachezaji wenye njaa ya ushindi, wanaojituma na kujivunia kuichezea Nigeria,"alisema kocha huyo, ambaye pia aliwahi kuinoa timu za taifa za Togo na Mali katika fainali hizo zinazotarajiwa kuanza Jumamosi nchini Afrika Kusini.

"Ni vizuri kuwaona wachezaji wakipambana kuwania namba kwenye kikosi changu cha kwanza. Hakuna mwenye namba ya kudumu, lazima wapambane kupata namba na kuendelea nayo," aliongeza kocha huyo.

Kwa upande wake, nahodha na beki wa kati wa timu hiyo, Joseph Yobo aliseme anataka kuifikia rekodi iliyowekwa na Nwankwo Kanu ya kuichezea timu hiyo fainali sita za Kombe la Mataifa ya Afrika.

"Kutwaa ubingwa itakuwa kazi ngumu, lakini naahidi tutafanya kila linalowezekana kuonyesha uwezo wetu. Nawaomba Wanigeria waendelee kutuombea dua na kuiamini timu yao,"alisema beki huyo wa zamani wa Everton,ambaye kwa sasa anacheza soka nchini Uturuki.

Yobo alisema wanakwenda Afrika Kusini kwa ajili ya kupeperusha benderaya taifa lao na kuongeza kuwa, hawatabweteka hadi watakapotimiza lengo lao.

"Bahati nzuri ni kwamba tunaye kocha anayetuelewa na nina hakika wachezaji wapo tayari kuitumikia nchi yao,"alisema.

Yobo alisema lengo lao la kwanza ni kuhakikisha wanafuzu hatua ya makundi na baada ya hapo,ndipo watakapoanza kufikiria hatua ya robo fainali, nusu fainali na kucheza fainali.

Nigeria imeshiriki fainali 10 za michuano hiyo katika miaka 50 iliyopita, imeshinda fainali mbili, imeshika nafasi ya pili mara nne na nafasi ya tatu mara saba.

No comments:

Post a Comment