KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, December 20, 2015

AZAM YAIKOSESHA RAHA MAJIMAJI


AZAM FC imepata ushindi muhimu wa ugenini, baada ya kuifunga mabao 2-1 Majimaji Uwanja wa Majimaji Songea jioni ya leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Ushindi huo unaifanya Azam FC ifikishe pointi 29 baada ya kucheza mechi 11 na kuendelea kubaki nafasi ya pili, nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 30 na mechi moja zaidi. 
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC, Didier Kavumbangu alianza kuifungia Azam FC dakika ya 10, kabla ya Ame Ally ‘Zungu’ kufunga la pili dakika ya 20.
Bao pekee la wenyeji, Majimaji lilifungwa na Alex Kondo dakika ya 55.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Serge Wawa, David Mwantika, Farid Mussa, Frank Domayo, Jean Mugiraneza, Ame Ally/Allan Wanga dk85, John Bocco na Didier Kavumbagu.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, JKT Ruvu imelazimishwa sare ya 2-2 na Coastal Union Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, wakati Mbeya City nayo imelazimishwa sare ya 1-1 na Mgambo JKT Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

MECHI ZIJAZO…
Desemba 23, 2015
Azam FC vs Mtibwa Sugar
Desemba 26, 2015
Ndanda FC vs JKT Ruvu
Yanga SC vs Mbeya City
Majimaji vs Prisons
Mwadui FC vs Simba SC
Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT
Coastal Union vs Stand United
Desemba 27, 2015
Azam FC vs Kagera Sugar
Toto Africans vs African Sports

IMETOLEWA BLOGU YA BINZUBEIRY

No comments:

Post a Comment