KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, November 8, 2015

LIGI Y SDL KUANZA NOVEMBA 15


Ligi Daraja la Pili nchini (SDL) inatarajiwa kuanza kutimua vumbi wikiendi ijayo Novemba 15 katika viwanja mbalimbali nchini, huku timu 24 zinazoshiriki ligi hiyo zikisaka nafasi nne za kupanda ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.

Makundi ya FDL ni kama ifuatvyo; Kundi A ni Abajalo FC (Tabora), Singida United (Singida), Mvuvuma FC (Kigoma), Milambo FC (Tabora), Green Warriors (Dar es Salaam) na Transit Camp (Dar es Salaam) wakati kundi B ni Bulyanhulu FC (Shinyanga), JKT Rwamkoma (Mara), Pamba FC (Mwanza), AFC Arusha, Madini FC (Arusha) na Alliance Schools (Mwanza).

Kundi C ni Kariakoo (Lindi), Mshikamano FC (Dar es Salaam), Cosmopolitan (Dar es Salaam), Abajalo FC (Dar es Salaam), Changanyikeni Rangers (Dar es Salaam) na Villa Squad (Dar es Salaam). Kundi D ni African Wanderers (Iringa), Mkamba Rangers (Morogoro), Town Small Boys (Ruvuma), Wenda FC (Mbeya), Coca-Cola Kwanza FC (Mbeya) na Sabasaba United (Morogoro).

No comments:

Post a Comment