KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, August 4, 2014

MISS TANZANIA 2012 KUSOMESHA ALBINO 50




Taasisi ya ya Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred ijulikanayo kwa jina na Brigitte Alfred Foundation (BAF) ikishirikiana na taasisi ya Junior Achievement Tanzania (JAT) inazindua rasmi mafunzo ya ujasiriamali kwa jamii ya Albino.

Akizungumza katika uzinduzi huo jana, Brigitte alisema kuwa taasisi yake kwa kushirikiana na JAT itaanza na mafunzo kwa albino 50.

Brigitte alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga sehemu kuu mbalimbali ambazo ni kujitambua (Life skills), kutathmini aina mbalimbali za biashara (Business Analysis), namna ya kutunza pesa ( How to save), kuandika mchanganuo wa biashara (Business Plan), kutembelea sehemu mbalimbali zinazoendana na biashara atakayoifanya na jinsi ya kuanza biashara.

Alisema kuwa BAF ikishirikiana na wadau mbalimbali na pia itagharimia gharama za mafunzo na mahitaji mbalimbali ya kuboresha hali yao.

“Mafunzo haya yatachukua muda wa mwaka mmoja yaani watashiriki na yataanza rasmi Agosti 18, kila mshiriki wa mafunzo haya atapatiwa kitabu chenye masomo yote ili aweze kuendelea kujisomea,” alisema Brigitte.

Mkurugenzi wa JAT, Maria Ngowi alisema kuwa wamejipanga kufanikisha mpango huo na wanaamini albino watakaopata mafunzo hayo watafanikiwa katika maisha yao ya kila siku. Ngowi alisema kuwa JAT imejikita katika Nyanja tatu ambazo ni ujasiria mali, elimu ya kuzalisha, kuiwekeza na kutunza fedha na elimu ya kazi.

Alisema kuwa taasisi yao ni sehemu ya taasisi kubwa ulimwenguni inayoitwa Junior Achievement International ambayo iko katika nchi 120 duniani huku afrika ikiwa katika nchi 17.

Kaimu Katibu Mkuu wa Tanzania Albino Society (TAS), Mohamed Chanzi alimshukuru Brigitte na JAT kwa kuwajali na kuomba wadau mbali mbali kuwaunga mkono.

“Wamelenga kutusaidia kimaisha, kwani msaada wa elimu ni mkubwa kulinganisha misaada mingine, naomba wadau wawaunge mkono,” alisema Chanzi

MICHUZI BLOGU KUDHAMINI MISS TEMEKE 2014



Washiriki wa Shindano la Miss Temeke 2014,wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye kambi yao ya Mazoezi iliyoanza rasmi Agosti 3,katika viwanja vya Chang'ombe,Jijini Dar es Salaam.Globu ya Jamii kwa kushirikiama na Michuzi Media Group wamejitosa kudhamini Shindano hilo,ambapo watatoa zawadi nono kwa mrembo atakaeshita taji la Miss Photogenic.

KIBA: SINA BIFU NA DIAMOND



MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ali Kiba amesema hana ugomvu wala bifu yoyote na msanii mwenzake nyota wa fani hiyo, Naseeb Abdul 'Diamond'.

Akizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania, kilichorushwa hewani na kituo cha televisheni cha TBC mwishoni mwa wiki, Kiba alisema amekuwa akishangazwa na taarifa hizo, ambazo zimekuwa zikiripotiwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari nchini.

"Mimi sina bifu au tatizo lolote na Diamond. Sielewi taarifa hizo zinatoka wapi,"alisema Kiba, ambaye ni msanii pekee nchini aliyewahi kurekodi nyimbo zake na baadhi ya wasanii maarufu duniani.

Kiba alisema uhusiano wake na Diamond ni mzuri kwa sababu wote ni wasanii na kila mmoja ana malengo yake katika fani ya muziki.

“ Namuheshimu sana, anaiwakilisha vyema nchi yetu, sielewi kwa nini watu wamekuwa wakizusha na kukuza vitu vya uongo. Nilidhani wangekuwa wamechoka, lakini bado tu wanazusha mambo kila kukicha,"alisema.

Hata hivyo, alikiri kuwa yeye si mpenzi wa nyimbo za Diamond na kusisitiza kuwa, haoni iwapo ana mpinzani katika fani hiyo hapa nchini.

Hivi karibuni, Kiba aliibuka na nyimbo mbili mpya, Mwana na Kimasomaso, ambazo zimeshaanza kushika chati katika vituo mbalimbali vya redio nchini na kuhusudiwa na mashabiki.

Kiba amerekodi nyimbo hizo baada ya kuwa kimya kwa zaidi ya miaka miwili, ukimya ambao ulikuwa ukitafsiriwa vibaya na mashabiki wake.

"Ni kweli kwamba nilikuwa kimya kwa muda mrefu, lakini si kwa sababu ambazo zimekuwa zikielezwa na watu mbalimbali. Ukimya wangu ulilenga kusoma mchezo unakwendaje na nitoke vipi,"alisema msanii huyo.

Kiba pia alikanusha madai kuwa, ukimya wake ulitokana na hali mbaya ya kifedha aliyokuwa nayo kutokana na nyimbo zake kutopokewa vyema na mashabiki kama alivyotarajiwa.

Kwa mujibu wa Kiba, video za nyimbo zake mpya zinatarajiwa kukamilika hivi karibuni kabla ya kuanza kuonyeshwa kwenye vituo mbalimbali vya televisheni.

Kiba alisema katika muziki, ni vizuri msanii kusoma mchezo mara kwa mara ili kujua utoke vipi badala ya kurudia kitu kile kile. Alisema ni muhimu kwa msanii kuwa mbunifu ili aweze kwenda na wakati.

Kabla ya kurekodi nyimbo hizo mbili mpya, Kiba aliwahi kutamba kupitia vibao vyake mbalimbali kama vile Cinderella, Mapenzi yanarun dunia, Single boy na Dushelele. Kibao cha Dushelele kiliweka rekodi ya kuuza nakala nyingi nchini na katika nchi jirani.

Sifa kubwa ya Kiba ni kutunga mashairi yenye mvuto na ujumbe mzuri kwa jamii, ikiwa ni pamoja na kutumia nahau na semi mbalimbali. Kwa mfano, katika wimbo wake mpya wa Kimasomaso, ametumia msemo maarufu unaosema 'Mwenda tezi na omo, marejeo ngamani.'

Kiba pia ni mwimbaji mwenye sauti nzuri na yenye mvuto, ikiwa ni pamoja na kuwa hodari wa kuwaburudisha mashabiki anapokuwa stejini. Ameshafanya ziara za kimuziki katika nchi nyingi duniani.

Mwaka 2011 alikwenda Marekani kurekodi wimbo na wanamuziki nyota wa Afrika. Alishiriki kurekodi wimbo huo uliotungwa na mwanamuziki nyota duniani, Robert Kelly akiwa na kina 2Face (Nigeria), Navio (Uganda), Amani (Kenya), Fally Ipupa (DRC), JK (Zambia),
4x4 (Ghana).

TAIFA STARS YATUPWA NJE NA MSUMBIJI KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA


Na Boniface Wambura, MAPUTO


KOCHA wa Taifa Stars, Mart Nooij amesema kwamba refa Mganda, Dennis Batte alikataa bao halali lililofungwa na John Bocco ‘Adebayor’ jana katika mchezo dhidi ya wenyeji Msumbiji, Uwanja wa Zimpeto mjini hapa.

Akizungumza baada ya mchezo huo ulioisha kwa Mambas kushinda 2-1 jana, Mholanzi huyo alilalamikia bao ambalo Taifa Stars ilifunga dakika ya 17 kupitia kwa Said Murad, lakini likakataliwa na mwamuzi Dennis Bate kutoka Uganda.

Aidha, Nooij amesema moja ya sababu za kikosi chake kupoteza mechi dhidi ya Mambas jana ni wachezaji wake kucheza kwa wasiwasi katika kipindi cha kwanza.

Taifa Stars iliruhusu bao la kwanza sekunde chache kabla ya kumalizika kipindi cha kwanza katika mechi ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kutafuta tiketi ya kucheza hatua ya makundi iliyochezwa leo (Agosti 3 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa wa Zimpeto hapa Maputo.

Bao hilo katika mechi hiyo iliyomalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya mabao 4-3 lilifungwa kwa kichwa na mshambuliaji Josemar Machaisse.

Nooij alisema wasiwasi katika kipindi cha kwanza ndio ulioipa Msumbiji fursa ya kutawala mechi hiyo katika kipindi hicho na kukimalizia ikiwa mbele kwa bao hilo la mshambuliaji huyo wa klabu ya Bravos de Maquis ya Angola.

Alisema timu yake ilitulia kipindi cha pili baada ya kumuingiza Amri Kiemba badala ya Khamis Mcha.

Aliongeza kuwa mchezaji Elias Pelembe aliyeifungia Msumbiji bao la pili dakika ya 83 kwa mpira wa adhabu nje ya eneo la hatari ndiye aliyemaliza mchezo huo.

Pia ni mchezaji huyo aliyebadili matokeo ya mchezo wa kwanza jijini Dar es Salaam ambapo Msumbiji ilisawazisha dakika tatu kabla ya filimbi ya mwisho.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, na ambayo ilicheza vizuri kipindi cha pili ilipata bao lake dakika ya 78 na Mbwana Samata kwa shuti la pembeni akiwa nje ya eneo la hatari na kumshinda kipa Dario Khan.

Matokeo hayo yameipeleka Msumbiji katika kundi C lenye timu za Cape Verde, Niger na Zambia. Mechi za hatua ya makundi kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco zitaanza kuchezwa mwezi ujao.

Katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.

Taifa Stars inarejea Dar es Salaam leo (Agosti 4 mwaka huu) saa 8 mchana kwa ndege ya Air Tanzania.

Friday, August 1, 2014

USAJILI WA WACHEZAJI LIGI KUU YA ENGLAND 2014/2015, NANI KAINGIA NANI KATOKA


 


ARSENAL
WALIOSAJILIWA
Alexis Sanchez (Barcelona, £30m),
Calum Chambers (Southampton, £12m),
Mathieu Debuchy (Newcastle, £10m),
David Ospina (Nice, £3m)

WALIOONDOKA
Thomas Eisfeld (Fulham, ada haikutajwa),
Bacary Sagna (Manchester City, huru),
Lukasz Fabianski (Swansea, huru),
Nicklas Bendtner (ameruhusiwa),
Park Chu-young (ameruhusiwa),
Chuks Aneke (ameruhusiwa),
Daniel Boateng (ameruhusiwa),
Wellington Silva (Almeria, mkopo),
Carl Jenkinson (West Ham, mkopo)

ASTON VILLA
WALIOSAJILIWA
Philippe Senderos (Fulham, huru),
Joe Cole (West Ham, huru),
Tom Leggett (Southampton, ada haikutajwa),
Isaac Nehemie (Southampton, ada haikutajwa)
Kieran Richardson (Fulham, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Marc Albrighton (Leicester City, huru),
Nathan Delfouneso (Blackpool, huru),
Jordan Bowery (Rotherham, ada haikutajwa),
Nicklas Helenius (Aalborg, mkopo),
Yacouba Sylla (Kayseri Erciyesspor, mkopo)

BURNLEY
WALIOSAJILIWA
Lukas Jutkiewicz (Middlesbrough, £2.5m),
Michael Kightly (Stoke, ada haikutajwa),
Marvin Sordell (Bolton, huru),
Matt Gilks (Blackpool, huru),
Matt Taylor (West Ham, huru),
Steven Reid (West Brom, huru)

WALIOONDOKA
Chirs Baird (West Brom, huru),
Junior Stanislas (Bournemouth, huru),
David Edgar (Birmingham, huru),
Keith Treacy (ameruhusiwa),
Brian Stock (ameruhusiwa),
Nick Liversedge (ameruhusiwa)

CHELSEA
WALIOSAJILIWA
Cesc Fabregas (Barcelona, £30m),
Diego Costa (Atletico Mdrid, £32m),
Mario Pasalic (Hadjuk Split, ada haikutajwa),
Filipe Luis (Atletico, £16m),
Didier Drogba (Galatasaray, huru)

WALIOONDOKA
David Luiz (Paris Saint-Germain, £50m),
Romelu Lukaku (Everton, £28million),
Samuel Eto'o (ameruhusiwa),
Frank Lampard (New York City, huru),
Sam Hutchinson (Sheffield Wednesday, huru),
Mark Schwarzer (ameruhusiwa),
Henrique Hilario (ameruhusiwa),
Wallace (Vitesse Arnhem, mkopo),
Bertrand Traore (Vitesse Arnhem, mkopo)
Thorgan Hazard (Borussia Monchengladbach, mkopo),
Ashley Cole (Roma, £1.5m),
Demba Ba (Besiktas, £8m),
Mario Pasalic (Elche, mkopo)
Patrick van Aanholt (Sunderland, ada haikutajwa),
Ryan Bertrand (Southampton, mkopo),
Gael Kakuta (Rayo Vallecano, mkopo)

CRYSTAL PALACE
WALIOSAJILIWA
Chris Kettings (Blackpool, huru)
Fraizer Campbell (Cardiff, £800k)

WALIOONDOKA
Jonathan Parr (Ipswich, huru),
Dean Moxey (Bolton, huru),
Aaron Wilbraham (Bristol City, huru),
Kagisho Dikgacoi (Cardiff, huru),
Danny Gabbidon (ameruhusiwa),
Neil Alexander (ameruhusiwa),
Ibra Sekajja (ameruhusiwa),
Alex Wynter (Portsmouth, mkopo),
Kwesi Appiah (Cambridge, mkopo),
Jose Campana (Sampdoria, ada haikutajwa),
Jack Hunt (Nottingham Forest, mkopo)

EVERTON
WALIOSAJILIWA
Romelu Lukaku (Chelsea, £28m),
Gareth Barry (Manchester City, free)
Muhamed Besic (Ferencvaros, £4m)

WALIOONDOKA
Apostolos Vellios, (Lierse, huru)
Mason Springthorpe (ameruhusiwa)
Magaye Gueye (Millwall, huru)

HULL
WALIOSAJILIWA
Robert Snodgrass (Norwich, £8m),
Jake Livermore (Tottenham, £6m),
Tom Ince (Blackpool, free),
Harry Maguire (Sheffield United, £2.5m),
Andrew Robertson (Dundee United, £2.85m)

WALIOONDOKA
Matty Fryatt (Nottingham Forest, huru),
Cameron Stewart (Ipswich, huru),
Robert Koren (ameruhusiwa),
Abdoulaye Faye (ameruhusiwa),
Conor Henderson (Crawley, huru),
Dougie Wilson (released),
Conor Townsend (Dundee United, mkopo),
Joe Dudgeon (Barnsley, mkopo)

LEICESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Matthew Upson (Brighton, huru),
Marc Albrighton (Aston Villa, huru),
Leonardo Ulloa (Brighton, £7m),
Ben Hamer (Charlton, huru),
Jack Barmby (Manchester United, huru),
Louis Rowley (Manchester United, huru)

WALIOONDOKA
Lloyd Dyer (Watford, huru),
Neil Danns (Bolton, huru),
Sean St Ledger (ameruhusiwa),
Zak Whitbread (Derby, huru),
Paul Gallagher (Preston, mkopo),
Marko Futacs (ameruhusiwa),
George Taft (Burton Albion, huru)

LIVERPOOL
WALIOSAJILIWA
Adam Lallana (Southampton, £23m),
Lazar Markovic (Benfica, £20m),
Emre Can (Bayer Leverkusen, £9.8m),
Rickie Lambert (Southampton, £4m)
Dejan Lovren (Southampton, £20m),
Divock Origi (Lille, £10m)

WALIOONDOKA
Luis Suarez (Barcelona, £75m),
Luis Alberto (Malaga, mkopo),
Iago Aspas (Sevilla, mkopo),
Andre Wisdom (West Brom, mkopo),
Divock Origi (Lille, mkopo)

MANCHESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Fernando (Porto, £12m),
Bacary Sagna (Arsenal, free),
Willy Caballero (Malaga, £6m),
Bruno Zuculini (Racing Club, £1.5m)

WALIOONDOKA
Costel Pantilimon (Sunderland, huru),
Joleon Lescott (West Brom, huru)
Gareth Barry (Everton, huru),
Alex Nimely (ameruhusiwa),
Rony Lopes (Lille, mkopo),
Emyr Huws (Wigan, mkopo)

MANCHESTER UNITED
WALIOSAJILIWA
Luke Shaw (Southampton, £31.5m),
Ander Herrera (Athletic Bilbao, £29m),
Vanja Milinkovic (FK Vojvodina, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Alexander Buttner (Dinamo Moscow, £5.6m),
Rio Ferdinand (QPR, huru),
Nemanja Vidic (Inter Milan, huru),
Federico Macheda (Cardiff City, huru),
Jack Barmby (Leicester, huru),
Louis Rowley (Leicester, huru)
Ryan Giggs (amestaafu),
Patrice Evra (Juventus, £2.5m)
Bebe (Benfica, £2.4m)

NEWCASTLE
WALIOSAJILIWA
Remy Cabella (Montpellier, £12m),
Emmanuel Riviere (Monaco, £6m),
Siem de Jong (Ajax, £6m),
Daryl Janmaat (Feyenoord, £5m),
Ayoze Perez (Tenerife, £1.5m),
Jack Colback (Sunderland, huru)

WALIOONDOKA
Mathieu Debuchy (Arsenal, £10m),
James Tavernier (Wigan, ada haikutajwa,
Dan Gosling (Bournemouth, huru),
Shola Ameobi (ameruhusiwa),
Conor Newton (Rotherham, huru),
Michael Richardson (ameruhusiwa),
Sylvain Marveaux (Guingamp, mkopo)

QUEENS PARK RANGERS
WALIOSAJILIWA
Rio Ferdinand (Manchester United, huru),
Steven Caukler (Cardiff, £8m)

WALIOONDOKA
Tom Hitchcock (Mk Dons, huru),
Aaron Hughes (Brighton, huru)
Stephane Mbia (ameruhusiwa),
Andrew Johnson (ameruhusiwa),
Luke Young (ameruhusiwa),
Hogan Ephraim (ameruhusiwa),
Angelo Balanta (ameruhusiwa),
Yossi Benayoun (Maccabi Haifa, ada haikutajwa),
Esteban Granero (Real Sociedad, ada haikutajwa)

SOUTHAMPTON
WALIOSAJILIWA
Dusan Tadic (Twente, £10.3m),
Graziano Pelle (Feyenoord, £8m),
Ryan Bertrand (Chelsea, loan)

WALIOONDOKA
Luke Shaw (Manchester United, £31.5m),
Rickie Lambert (Liverpool, £4m),
Adam Lallana (Liverpool, £23m)
Guly do Prado (released),
Lee Barnard (Southend, huru),
Jonathan Forte (released),
Danny Fox (Nottingham Forest, huru),
Andy Robinson (Bolton, huru),
Tom Leggett (Aston Villa, ada haikutajwa),
Isaac Nehemie (Aston Villa, ada haikutajwa)
Dejan Lovren (Liverpool, £20m)
Calum Chambers (Arsenal, £12m)

STOKE CITY
WALIOSAJILIWA
Mame Biram Diouf (Hannover, huru),
Dionatan Teixeira (Banska Bystrica, ada haikutajwa),
Phil Bardsley (Sunderland, huru),
Steve Sidwell (Fulham, huru),
Bojan Krkic (Barcelona, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Michael Kightly (Burnley, ada haikutajwa),
Matthew Etherington (ada haikutajwa),
Juan Agudelo (ada haikutajwa)

SUNDERLAND
WALIOSAJILIWA
Billy Jones (West Brom, huru),
Jordi Gomez (Wigan, huru),
Costel Pantilimon (Manchester City, huru)
Patrick van Aanholt (Chelsea, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Jack Colback (Newcastle, huru),
Craig Gardner (West Brom, huru),
Phil Bardsley (Stoke, huru),
Billy Knott (Bradford, huru)
Keiren Westwood (Sheffield Wednesday, huru),
Carlos Cuellar (ameruhusiwa),
Andrea Dossena (ameruhusiwa),
Louis Laing (ameruhusiwa),
Oscar Ustari (Newell's, huru),
David Vaughan (Nottingham Forest, huru),
John Egan (Gillingham, huru),
Ignacio Scocco (Newell's, £800,000)

SWANSEA
WALIOSAJILIWA
Marvin Emnes (Middlesbrough, £1.5m),
Bafetimbi Gomis (Lyon, huru),
Lukasz Fabianski (Arsenal, huru),
Stephen Kingsley (Falkirk, ada haikutajwa),
Gylfi Sigurdsson (Tottenham, ada haikutajwa)
Jefferson Montero (Monarcas Morelia, £4m)

WALIOONDOKA
Leroy Lita (ameruhusiwa),
David Ngog (ameruhusiwa),
Daniel Alfei (Northampton, mkopo),
Jernade Meade (ameruhusiwa),
Darnel Situ (ameruhusiwa),
Michu (Napoli, mkopo),
Ben Davies (Tottenham, £10m)
Michel Vorm (Tottenham, £5m)
Alejandro Pozuelo (Rayo Vallecano, ada haikutajwa)

TOTTENHAM
WALIOSAJILIWA
Ben Davies (Swansea, ada haikutajwa)
Michel Vorm (Swansea, £5m)

WALIOONDOKA
Jake Livermore (Hull, £6m),
Heurelho Gomes (Watford, huru),
Cameron Lancaster (ameruhusiwa),
Alex Pritchard (Brentford, mkopo),
Gylfi Sigurdsson (Swansea, mkopo)

WEST BROMWICH ALBION
WALIOSAJILIWA
Brown Ideye (Dynamo Kiev, £10m),
Craig Gardner (Sunderland, huru),
Joleon Lescott (Manchester City, huru),
Chris Baird (Burnley, huru),
Sebastien Pocognoli (Hannover 96, ada haikutajwa),
Andre Wisdom (Liverpool, mkopo)

WALIOONDOKA
Liam Ridgewell (Portland Timbers, huru),
Billy Jones (Sunderland, huru),
Steven Reid (Burnley, huru),
Cameron Gayle (Shrewsbury, huru),
Diego Lugano (ameruhusiwa),
Zoltan Gera (ameruhusiwa),
Scott Allan (ameruhusiwa),
Nicolas Anelka (ameruhusiwa),
George Thorne (Derby County, ada haikutajwa)

WEST HAM
WALIOSAJILIWA
Enner Valencia (Pachuca, £12m),
Cheikhou Kouyate (Anderlecht, £7m),
Mauro Zarate (Velez Sarsfield, ada haikutajwa),
Aaron Cresswell (Ipswich, ada haikutajwa),
Diego Poyet (Charlton, ada haikutajwa),
Carl Jenkinson (Arsenal, huru)

WALIOONDOKA
Joe Cole (Aston Villa, huru),
Matt Taylor (Burnley, huru),
Stephen Henderson (Charlton, huru),
Jack Collison (ameruhusiwa),
George McCartney (ameruhusiwa),
Callum Driver (ameruhusiwa),
Jordan Spence (ameruhusiwa),

Thursday, July 31, 2014

AZAM ACADEMY BINGWA KOMBE LA ROLLINGSTONE



AZAM FC imetwaa ubingwa wa michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 20 kwa nchi za Maziwa Makuu, maarufu kama Rollingston baada ya kuichapa timu ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) ya Mgulani Twalipo bao 2-0 katika fainali jioni hii Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

Jamil Mchaulu ‘Balotelli’ aliyefunga bao la kwanza dakika ya tatu, baada ya kuwatoka vizuri beki wa kulia wa Twalipo, Ally Mbonde na beki wa kati Ally Athumani kisha kumtungua kipa wao, Kulwa Baumba.


Twalipo ilipoteza mwelekeo mapema tu baada ya bao hilo, na wachezaji wake kuanza kucheza rafu nyingi, badala ya kutengeneza mipangop ya kusawazisha bao.

Azam walitumia mwanya huo kucheza mpira wa kuachiana pasi za haraka uwanjani kuwakwepa ‘wapiga kiatu’ wa jeshini na kufanikiwa kumaliza dakika 45 za kwanza wakiwa wanaongoza 1-0.

Kipindi cha pili, mchezo ulizidi kunoga, Twalipo wakisaka bao la kusawazisha na Azam wakitafuta mabao zaidi- hali iliyosababisha mashambulizi ya pande zote mbili.

Alikuwa ni Adam Omar Soba aliyeihakikishia Kombe la kwanza la Rollingston Azam FC baada ya kufunga bao la pili dakika ya 88.

Katika mchezo wa kwanza wa kuwsaka mshindi wa tatu, Champion ya Kawe ilitwaa ubingwa wa U17 kwa kuifunga Bom Bom ya Ilala kwenye Uwanja huo huo, Karume.

TAIFA STARS YAENDA AFRIKA KUSINI



Msafara wa watu 27 wa kikosi cha timu ya Taifa (Taifa Stars) kimeondoka nchini juzi saa 10 jioni kwa ndege ya Air Tanzania kwenda Afrika Kusini ambapo kitapiga kambi ya siku mbili kabla ya kuingia Maputo kuikabili Msumbiji (Mambas).

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iliwasili Afrika Kusini saa 9 asubuhi jana kwa ndege ya Fastjet, na baadaye jioni kuunganisha safari ya Afrika Kusini.

Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika dhidi ya Msumbiji itachezwa Agosti 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa uliopo Zimpeto nje kidogo ya Jiji la Maputo.

Msafara huo wa Taifa Stars kwenda Afrika Kusini unajumuisha wachezaji 19 na waliobaki ni maofisa wa Benchi la Ufundi lililo chini ya Kocha Mkuu Mart Nooij kutoka Uholanzi.

Wakati kiungo Mwinyi Kazimoto ametua leo (Julai 29 mwaka huu) nchini kuungana na wenzake, washambuliaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wao wataungana na wenzao kesho (Julai 30 mwaka huu) jijini Johannesburg wakitokea Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Wakati huo huo, Serengeti Boys imewasili salama jana (Julai 28 mwaka huu) jijini Johannesburg, Afrika Kusini kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 dhidi Afrika Kusini (Amajimbos).

Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili itachezwa Jumamosi, Agosti 2 mwaka huu kwenye Uwanja wa Dobsonville uliopo Soweto kuanzia saa 9 kamili mchana kwa saa za Afrika Kusini.

Timu hizo zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyofanyika Julai 18 mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam. Serengeti Boys inahitaji ushindi kwenye mechi hiyo au aina yoyote ya sare ya mabao ili ifuzu kwa raundi ya tatu.

Monday, July 28, 2014

MANJI AUNDA KAMATI MPYA YA UTENDAJI YANGA, AMUINGIZA KUNDINI TARIMBA ABBASI


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:

1. Mwenyekiti na Makamo Mwenyekiti wa Klabu ya Young Africans Sports Club (YANGA) kwa
mamlaka waliyopewa na Wanachama,kubadilisha, kupunguza au kuongeza Mjumbe yeyote kwenye
Kamati ya Utendaji wakati wowote,kulingana na changamoto wanazoziona zinazoikabili Klabu ya
YANGA, Mwenyekiti na Makamo Mwenyekiti wa YANGA wanapenda kutoa taarifa rasmi, kuwa
Kamati ya Utendaji ya YANGA na Kamati zote ambazo ziko chini ya Kamati ya Utendaji zitavunjwa
kuanzia tarehe 31 Julai, 2014.

2.Vile vile, Mwenyekiti na Makamo Mwenyekiti wa YANGA wanapenda kuwashukuru Wajumbe wote
wa Kamati ya Utendaji ya YANGA kwa juhudi zao za kutekeleza shughuli za Klabu.

3. Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Klabu ya YANGA Bw.Yusuf Manji na naibu wake Bw.Clement

Sanga wanatangaza Kamati ya Utendaji mpya ya Young Africans Sports Club ambayo itakuwa
madarakani kuanzia 1 Agosti, 2014 kama inavyoelezwa na kila Mjumbe anavyotajwa hapo chini anakuwa
na majukumu ya msingi ya kusimamia kama inavyoonyeshwa pembeni ya jina lake.

WAJUMBE WAPYA WA KAMATI YA UTENDAJI YA YANGA NI HAWA WAFUATAO:
1.Bw.Abubakar Rajabu - Mradi wa Jangwani City
2.Bw.Sam Mapande - Sheria na Utawala Bora
3.Bw.George Fumbuka - Uundwaji wa Shirika
4.Bw.Waziri Barnabas - Vibali vya Hatimiliki na Mahusiano na Wafadhili
5.Bw.Abbas Tarimba - Mipango na Uratibu
6.Bw.Isaac Chanji na Bw.Seif Ahmed - Uendelezaji wa Mchezo
7.Bw.Musa Katabalo - Mauzo ya Bidhaa
8.Bw.Mohammed Bhinda - Ustawishaji wa Matawi
9.Bw.David Ndeketela Sekione - Uongezaji wa Wanachama
10.Bw.Mohammed Nyenge - Utangazaji wa Habari, Taarifa, Matangazo n.k.

WAJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI ILIYOUNDWA UPYA WATASIMAMIA KIMSINGI
KAMATI NDOGO ZIFUATAZO:
•Kamati ya Maadili - Bw.Sam Mapande
•Kamati ya Nidhamu - Bw.Sam Mapande
•Kamati ya Uchaguzi - Bw. Sam Mapande
•Kamati ya Uchumi na Fedha - Bw.George Fumbuka na Bw.Waziri Barnabas
•Kamati ya Mashindano - Bw.Seif Ahmed & Bw.Isaac Chanji
•Kamati ya Soka la Vijana na Wanawake - Bw.Seif Ahmed &Bw.Isaac Chanji
•Kamati ya Ufundi - Bw.Seif Ahmed &Bw.Isaac Chanji

5. Mwenyekiti na Makamo Mwenyekiti wa YANGA wanamategemeo makubwa kuwa waliotajwa hapo
juu watahakikisha wana timiza malengo yaliyokusudiwa na YANGA ili“DAIMA MBELE, NYUMA
MWIKO” mpaka hapo itakapoamuliwa kubadilishwa au kutenguliwa vinginevyo.

6. Mwisho,tunawaomba ushirikiano wa dhati ili kuhakikisha kuwa YANGA inapiga hatua mbele na
inafanikiwa katika kufikia malengo na mipango yake ya maendeleo ya muda mfupi na ya muda mrefu
kwa manufaa ya Klabu, Timu na wana YANGA popote walipo duniani.

“MUNGU AIBARIKI YANGA.”
(BENO NJOVU)
KATIBU MKUU- YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB.

AZAM YATINGA FAINALI KOMBE LA ROLLINGSTONE,YAWATOA WABABE WA YANGA




AZAM FC imeingia fainali ya michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 20 kwa nchi za Maziwa Makuu, maarufu kama Rollingston baada ya kuifunga mabao 2-0 EMIMA, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.


Kwa matokeo hayo, Azam FC iliyoitoa Simba SC katika Robo Fainali, itakutana na Twalipo katika fainali ya timu za Manispaa ya Temeke tupu kesho Chamazi.

EMIMA iliyoitoa Yanga SC katika hatua ya 16 Bora na Mwambao ya Bagamoyo mkoani Pwani katika Robo Fainali, leo ilimalizwa mapema tu kipindi cha kwanza na Azam FC.

Jamil Mchaulu ‘Balotelli’ ndiye aliyeifungisha virago timu hiyo ya Tabata kwa mabao yake dakika za 18 na 44 na kufikisha jumla ya mabao matatu katika mashindano haya.

Kocha Mkuu wa Azam FC, Mcameroon Joseph Marius Omog kama kawaida yake alikuwepo uwanjani kuangalia vipaji vya akademi na baada ya mechi akasema; “Nina furaha, huu ni msingi mzuri kwetu, vipaji na uwezo katika akademi, inafurahisha sana,”alisema Omog.

Mapema katika Nusu Fainali ya kwanza, Twalipo iliitoa Ashanti United ya Ilala kwa bao 1-0, Uwanja huo huo wa Azam Complex.

Dakika 90 za mchezo huo zilimalizika bila bao na ilibaki moja tu kutimia dakika 30 za nyongeza mchezo uhamie kwenye penalti kuamua mshindi, lakini Suleiman Bofu akamaliza kazi.

Mshambuliaji huyo hatari alimalizia shambulizi la kushitukiza kuipatia bao lililoipeleka fainali Twalipo.

EMIMA na Ashanti zitamenyana katika mchezo wa kusaka mshindi wa tatu pia kesho Chamazi.

AZAM YAITOA SIMBA KOMBE LA ROLLINGSTONE



AZAM FC imetinga Nusu Fainali ya michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 20 kwa nchi za Maziwa Makuu, Rollingston baada ya kuitoa Simba SC, zote za Tanzania kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.


Makocha wakuu wa vikosi vya kwanza vya timu hizo za Dar es Salaam, Mcameroon Joseph Marius Omog wa Azam ya Chamazi na Mcroatia Zdravko Logarusic wa Simba ya Msimbazi wote walikuwepo kushuhudia mchezo huo.

Shujaa wa Azam FC alikuwa ni kipa wao, Hamad Juma aliyepangua penalti mbili za wachezaji wa Simba SC, Dadi Yunus na Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ wakati penalti ya Haruna Abdallah iliota mbawa.

Waliofunga penalti za Simba SC ni Ibrahim Hajibu na Omary Hussein wakati penalti za Azam zilifungwa na Kassim Kisengo, Reyna Mngungila na Adam Omar.

Kipa wa timu ya taifa ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Peter Manyika alipangua penalti mbili pia za Shirazy Abdallah na Masoud Abdallah, lakini akaangushwa na wachezaji wake waliokosa penalti.

Kipa wa Azam FC, Hamad Juma alichomoka kwa shangwe baada ya kupangua mkwaju wa mwisho wa Tshabalala aliyesajiliwa kwa ajili ya kikosi cha kwanza cha Simba SC kutoka Kagera Sugar msimu huu.

Peter Manyika aliyefanya kazi nzuri ya kuokoa michomo mingi ya hatari ndani ya dakika 90 na akaenda kucheza penalti mbili baadaye aliangua kilio baada ya mchezo huo.

Kwa ujumla mchezo ulikuwa mzuri na timu zote zilishambuliana kwa zamu, huki wachezaji wakionyesha vipaji vya hali ya juu. Kwa kutolewa, Simba SC imeungana na watani wao, Yanga SC ambao jana walitolewa katika hatua ya 16 Bora. Nusu Fainali zinatarajiwa kuchezwa kesho.

Sunday, July 27, 2014

SERENGETI BOYS KWENDA AFRIKA KUSINI KESHO



Msafara wa watu 25 wa kikosi cha timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) unaondoka kesho (Julai 28 mwaka huu) kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya mechi dhidi ya Afrika Kusini (Amajimbos).

Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya pili itachezwa Jumamosi, Agosti 2 mwaka huu kwenye Uwanja wa Dobsonville uliopo Soweto, Johannesburg kuanzia saa 9 kamili mchana kwa saa za Afrika Kusini.

Timu hizo zilitoka suluhu katika mechi ya kwanza iliyofanyika Julai 18 mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam. Mshindi atacheza raundi ya mwisho ya michuano hiyo ya Afrika na mshindi wa mechi kati ya Misri na Congo Brazzaville.

Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitafanyika mwakani nchini Niger.

Wachezaji wanaounda kikosi cha Serengeti Boys katika msafara huo utakaoondoka saa 2 usiku kwa ndege ya Fastjet ni Abdallah Jumanne Shimba, Abdulrasul Tahil Bitebo, Abutwalibu Hamidu Msheri, Adolf Mtsigwa Bitegeko, Ally Aziz Mnasi, Ally Shaban Mabuyu na Athanas Enemias Mdamu.

Wengine ni Badru Haji Othman, Baraka Yusuph Baraka, Issa Backy Athuman, Juma Ally Yusuph, Kelvin Longnus Faru, Martin Kiggi Luseke, Metacha Boniface Mnata, Mohamed Mussa Abdallah, Omary Ame Omary, Omary Natalis Wayne, Prospal Alloyce Mushin na Seif Said Seif.

Benchi la Ufundi linaongozwa na Kocha Mkuu Hababuu Ally Omary akisaidiwa na Stewart John Hall (Mshauri wa Ufundi), Peter Manyika (Kocha wa makipa), Richard Yomba (Daktari), na Edward Venance (Mtunza vifaa).

Msafara wa timu hiyo itakayorejea nyumbani Agosti 4 mwaka huu unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Khalid Mohamed Abdallah.

Wednesday, July 23, 2014

JAMES RODRIGUEZ ATAMBULISHWA RASMI REAL MADRID




 
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Colombia, James Rodriguez, juzi alitambulishwa rasmi na klabu yake mpya ya Real Madrid ya Hispania.

James amemwaga wino wa kuichezea Real Madrid kwa miaka sita na uhamisho wake umeigharimu klabu hiyo pauni milioni 60 za Uingereza na kuwa mchezaji ghali wa nne duniani.

Maelfu ya mashabiki wa Real Madrid walifurika kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu wakati nyota huyo wa Kombe la Dunia alipokuwa akitambulishwa na Rais wa klabu hiyo, Florentino Perez.

Utambulisho huo uliingia doa baada ya shabiki mmoja, anayesadikiwa kuwa ni kutoka Colombia, alipovamia ndani ya uwanja na kwenda moja kwa moja kumkumbatia James kabla ya kutolewa na polisi.

Rekodi ya mchezaji ghali duniani kwa sasa inashikiliwa na Gareth Bale, ambaye uhamisho wake uliigharimu Real Madrid pauni milioni 80, akifuatiwa na Cristiano Ronaldo, aliyenunuliwa pia kwa pauni milioni 80. Luis Suarez anashika nafasi ya tatu kutokana na uhamisho wake kuigharimu Barcelona pauni milioni 75.

Real Madrid imemuhamisha James kutoka Monaco ya Ufaransa. Wakati wa utambulisho wake, Perez alimpeleka mchezaji huyo kwa nyota wa zamani wa klabu hiyo, Alfredo Di Stefano, ambaye pia alihamishwa kutoka Colombia.

WACHEZAJI 10 GHALI DUNIANI
£80m - Gareth Bale (Tottenham to Real Madrid)
£80m - Cristiano Ronaldo (Manchester United to Real Madrid)
£75m - Luis Suarez (Liverpool to Barcelona)
£60m - James Rodriguez (Monaco to Real Madrid)
£59m - Zlatan Ibrahimovic (Inter Milan to Barcelona)
£56m - Kaka (AC Milan to Real Madrid)
£55m - Edinson Cavani (Napoli to PSG)
£51m - Radamel Falcao (Atletico Madrid to Monaco)
£50m - Fernando Torres (Liverpool to Chelsea)
£50m - David Luiz (Chelsea to PSG)

YANGA KUFUNGUA DIMBA NA RAYON KOMBE LA KAGAME


YANGA imepangwa kufungua dimba la michuano ya soka ya Kombe la Kagame kwa kumenyana na wenyeji, Rayon Sports kwenye dimba la Amahoro mjini Kigali.


Ratiba ya michuano hiyo iliyotolewa juzi na Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), inaonyesha kuwa mechi hiyo itapigwa Agosti 8 mwaka huu.

Wawakilishi hao wa Tanzania Bara wamepangwa kundi A pamoja na timu za Rayon, Coffee ya Ethiopia, Atlabara ya Sudan Kusini na KMKM ya Zanzibar.

Kundi B litakuwa na timu za APR ya Rwanda, KCC ya Uganda, Flambeau Del Est ya Burundi, Telecom ya Djibouti na Gor Mahia ya Kenya.

Timu zilizopangwa kundi C ni Vital'O ya Burundi, El Merreikh ya Sudan, Police ya Rwanda na Banadir ya Ethiopia.

Kwa mujibu wa ratiba, mbali na mechi ya ufunguzi kati ya Yanga na Rayon, mechi zingine za ufunguzi zitazikutanisha Atlabara na KMKM na kati ya Gor Mahia na KCC.

DIARA AONGOZA KWA MABAO AZAM


MSHAMBULIAJI Ismaila Diara kutoka Mali ameendelea kufanya vizuri zaidi ya wachezaji wenzake wapya wa kigeni kwa kufunga mabao Azam FC.

Azam FC imesajili washambuliaji wapya watatu wa kigeni, Didier Kavumbangu kutoka Burundi, Leonel Saint-Ptreux kutoka Haiti na Diara wanaoungana na Kipre Herman Tchetche wa Ivory Coast, kinara wa mabao wa timu hiyo kwa misimu miwili iliyopita.

Diara jana alifikisha jumla ya mabao matatu aliyoifungia Azam FC katika michezo mitatu ya kujipima nguvu aliyoichezea akifunga bao moja katika ushindi wa 2-1 dhidi ya timu ya Daraja la Kwanza, Friends Rangers.

Bao lingine la Azam FC, lilifungwa na Gaudence Mwaikimba wakati bao la kufutia machozi la Rangers lilifungwa na Yussuf Mgwao.

Awali, Diara aliifungia Azam FC mabao mawili katika ushindi wa 3-2 dhidi ya kombaini ya Jeshi, bao lingine likifungwa na Mudathir Yahya.

Leonel ana bao moja tu alilofunga dhidi ya Polisi Morogoro katika ushindi wa 1-0, wakati Kavumbangu ana bao moja pia alilofunga katika ushindi wa 2-1 dhidi ya JKT Ruvu, bao lingine likifungwa na Kipre Tchetche.

Azam FC leo itaendelea na mazoezi Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam wakati kesho itacheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja huo.

VODACOM KUDHAMINI ZIARA YA ZIARA YA REAL MADRID


VODACOM Tanzania ni miongoni mwa makampuni yaliyojitokeza kudhamini ziara kikosi cha wachezaji nyota waliowahi kutamba Real Madrid ya Hispania, maarufu kama Real Madird Legends ambao watazuru nchini mwezi ujao.


Meneja ziara ya magwiji wa Real Madrid, Dennis Ssebo amewaambia Waandishi wa Habari asubuhi ya leo katika hoteli ya New Africa, Dar es Salaam kwamba, mbali na Vodacom, wadhamini wengine wa ziara hiyo ni Fastjet, Tropical, Pembe Flower, Lake Gas, EFM Radio na Ladger Plaza Bahari Beach.

Wachezaji waliotamba kuanzia La Liga, wakacheza ligi nyingine za Ulaya, Kombe la Ulaya, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia waliowahi kuchezea Madrid watakuja nchini Agosti 22.

Katika ziara hiyo, pamoja na kucheza mchezo wa kirafiki na kikosi maalum cha wachezaji nyota wa Tanzania, pia watafanya utalii katika vivutio mbalimbali, ikiwemo kupanda mlima Kilimanjaro.

Real Madrid inakuja nchini kwa mwaliko wa kampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini ya Mkurugenzi wake Mkuu, Farough Baghozah.

Miongoni mwa nyota wanaotarajiwa kuja na Real nchini ni pamoja na Wanasoka Bora wa zamani wa Dunia, Mfaransa Zinadine Zidane, Mreno Luis Figo na Mbrazil, Ronaldo Lima.

Magwiji hao wa Real tayari wamekwishafanya matangazo ya ziara yao nchini wakisema wana hamu mno ya kukanyaga ardhi ya Tanzania.

LOGA AMWAGA WINO SIMBA MIAKA MIWILI


KOCHA Mkuu wa Simba SC, Mcroatia Zdravko Logarusic amesaini Mkataba mpya wa mwaka mmoja na kusema kwamba timu hiyo itakuwa bora msimu ujao, ubingwa wa Ligi Kuu ikiwa lengo la kwanza.


Akizungumza makao makuu ya klabu, Mtaa wa Msimbazi baada ya kusaini Mkataba huo, kocha huyo wa zamani wa Gor Mahia ya Kenya amesema kwamba amefurahi kusaini kandarasi mpya na sasa anaelekeza nguvu zake kwenye kazi.

Loga amesema Simba SC itakuwa timu bora msimu ujao na lengo lake kuu ni kuhakikisha inatwaa ubingwa.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais Simba, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ aliyesaini Mkataba na kocha huyo amesema kwamba sasa msalaba mkubwa wa Loga ni kuhakikisa Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu msimu ujao linatua Msimbazi.

Kaburu pia amesema Kocha Msadizi, Suleiman Matola ‘Bin Laden’ naye alisaini Mkataba wa miaka miwili tangu Novemba mwaka jana.

Loga alijiunga na Simba SC Desemba mwaka jana kwa Mkataba wa miezi sita, lakini uongozi wa klabu hiyo umeridhishwa na kazi yake na kumuongeza mwaka mmoja mwingine.

Tuesday, July 22, 2014

USAJILI LIGI KUU WAONGEZWA KWA WIKI MBILI


Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeongeza muda wa usajili kwa wiki mbili ili kuzipa klabu nafasi ya kukamilisha taratibu zinazotakiwa. Hivyo hatua ya kwanza ya usajili inakamilika Agosti 17 mwaka huu badala ya Agosti 3 ya awali.

Kutokana na marekebisho hayo, kipindi cha uhamisho kinakamilika Agosti 17 mwaka huu wakati pingamizi itakuwa kati ya Agosti 19 hadi 26 mwaka huu.

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji itathibitisha usajili kati ya Septemba 1 na 2 mwaka huu.

Uhamisho wa kimataifa, usajili wa wachezaji huru, na utatuzi wa dosari za usajili unatakiwa uwe umekamilika kufikia Septemba 7 mwaka huu. Uthibitisho wa hatua ya mwisho ya usajili utafanywa Septemba 15 mwaka huu.

Kwa upande wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2014/2015 itaanza Septemba 20 mwaka huu, na ratiba itatolewa mwezi mmoja kabla ya kuanza ligi hiyo.

TAIFA STARS KUWEKA KAMBI MBEYA NA AFRIKA KUSINI



Kikosi cha Taifa Stars kinatarajia kuondoka keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Mbeya ambapo kitapiga kambi ya wiki moja kujiandaa kwa mechi ya marudiano dhidi ya Msumbiji.

Mechi hiyo ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kutafuta tiketi ya kushiriki Fainali za Afrika (AFCON) zitakazochezwa mwakani nchini Morocco itafanyika wikiendi ya Agosti 2 na 3 mwaka huu nchini Msumbiji.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka nchini Julai 31 mwaka huu kwenda Johannesburg, Afrika Kusini ambapo itafanya mazoezi ya mwisho kabla ya kutua Maputo kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa wa Zimpeto.

…MECHI YAINGIZA SHILINGI MILIONI 158
Mechi ya michuano ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Msumbiji (Mambas) iliyochezwa juzi (Julai 20 mwaka huu) imeingiza sh. 158,350,000 kutokana na washabiki 19,684 walioingia kwa kiingilio cha sh. 7,000 na sh. 30,000.

Mgawo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 24,155,084.75, gharama za tiketi (MaxMalipo) sh. 19,684,000, gharama za mchezo sh. 22,902,183, uwanja sh. 11,451,092, Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 5,725,546 na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 74,432,095.

Tunawashukuru washabiki wote waliojitokeza kwenye Uwanja wa Taifa kuishangilia Taifa Stars katika mechi hiyo iliyomalizika kwa sare ya mabao 2-2.

STEVEN GERRARD ATANGAZA KUSTAAFU SOKA YA KIMATAIFA



Asema Beckham, Rooney na Terry walikuwa wachezaji bora aliowahi kucheza nao England.
Asema alicheza na wachezaji wenye kiwango cha juu kwenye kikosi cha England
Awataja Beckham, Rooney, Terry, Lampard na Scholes kuwa ni wachezaji aliokuwa akipenda kuchati nao kwenye chumba cha wachezaji
Nahodha huyo wa Liverpool alisema Beckham, aliyestaafu soka 2013, alimsaidia kufikia uamuzi wa kustaafu soka ya kimataifa.
Asema Kocha Roy Hodgson alimruhusu kutimiza ndoto aliyokuwa nayo tangu akiwa mdogo ya kuvaa kitambaa cha unahodha wa England
Ameuelezea uamuzi wake wa kustaafu soka ya kimataifa kuwa ulikuwa mgumu katika maisha yake kisoka
Gerrard asema kwa sasa akili yake ipo kwenye klabu ya Liverpool, kuliko kujiunga na klabu nyingine
Tayari Gerrard anayo leseni ya ukocha na sasa anapigania kupata daraja C
Ana hakika atafanya tena kazi kwenye kikosi cha England katika miaka kati ya 20 hadi 40 ijayo.




Monday, July 21, 2014

TFF YAIOMBA AIRTEL KUDHAMINI UNDER 20




Meneja Mutukio wa Airtel Tanzania Rebeca Mauma akizungumza wakati wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars iliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Baadhi ya washiriki wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars wakifutilia kwa makini moja ya mada zilizowasilishwa kwenye semina hiyo iliyofanyika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Katibu mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa akisisitiza jambo wakati wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars iliyofanyika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando akiteta na Katibu Mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa wakati wa semina elekezi ya Airtel Rising Stars iliyofanyika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF Salum Madadi na Mwenyekiti wa DRFA Almasi Kasongo.


Katibu Mkuu wa shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) Selestine Mwesigwa amesisitiza umuhimu wa programu za vijana kwa maendeleo ya soka nchini na kuitaka kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kuangalia uwezekano wa kuwa wadhamini wa timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20.

Akifungua semina elekezi kwa makatibu wakuu wa mikoa inayoshiriki mashindano ya vijana ya Airtel Rising Stars (ARS) iliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Jumamosi Julai 19, 2014 Mwesigwa alisema hali halisi inaonyesha kwamba miaka michache ijayo wachezaji wengi watakaounda timu ya taifa ya U-20 watatokana na ARS hivyo ni vema kampuni ya Airtel ikawa mdhamini mkuu wa timu hiyo.

Alisema kuwa suala la programu za vijana ni agenda namba moja ya TFF na kuzitaka timu za ligi kuu kuzingatia maagizo ya shirikisho hilo la kuwa na timu za vijana. “Klabu ya Simba imefanikiwa sana katika suala hili na ni vema timu nyingine za ligi kuu zikaiga mfano huo”, alisema Mwesigwa na kuipongeza Airtel kwa kuwekeza katika soka la vijana.

“Wachezaji wanapolelewa na klabu tangu wakiwa wadogo inakuwa ni rahisi kwao kuendana na maadili ya klabu hiyvo kuwa na wachezaji wenye nidhamu ya hali ya juu tofauti na wachezaji waosajiliwa kutoka sehemu mbali mbali wakiwa na umri mkubwa”, alisema.

Aliwataka makatibu hao wa mikoa kuzingatia kanuni ikiwa ni pamoja na umri ili kuwafanya vijana watakaoshiriki mashindano ya Airtel Rising Stars kuwa na ushindani ulio sawa. Mashindano ya ARS yanashirikisha vijana chini ya umri wa miaka 17.

Mwesigwa aliungwa mkono na Mwenyekiti wa kamati ya vijana ya TFF Ayoub Nyenzi aliyesema kuwa programu za vijana e.g. ARS ndiyo mkombozi wa kweli wa soka popete pale duniani.

Mashindano hayo yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi katika ngazi ya mkoa Julai 27 na kushirikisha mikoa ya Mbeya, Morogoro, Mwanza, Ilala, Kinondoni na Temeke kwa upande wa wavulana huku timu za wasichana zikitoka mikoa ya Mwanza, Mbeya, Zanzibar, Ilala, Kinondoni na Temeke.

Akiongea katika semina hiyo Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson Mmbando aliwapongeza viongozi wa mikoa kwa kazi nzuri iliyoiwezesha Tanzania kutwaa ubingwa wa mashindano ya kimataifa ya ARS (wasichana) yaliyofanyika Nigeria na kuzawadiwa USD 10,000, medali na vikombe.

“Vile vile timu ya wavulana ilifanya vizuri sana na ni imani yangu kwamba mwaka huu Tanzania itashinda vikombe kwa wasichana na wavulana”, alisema na kusisitiza nia thabiti ya Airtel kuendelea kuboresha mashindano hayo.

Naye Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF Salum Madadi aliwataka makatibu hao kufanyakazi kwa karibu na kamati ya vijana ya TFF inayosimamia mashindano hayo