'
Friday, October 19, 2012
MTANZANIA AOMBEWA ITC MAREKANI
Mchezaji Millan Mbise kutoka Tanzania ameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) itakayomwezesha kucheza mpira wa miguu nchini Marekani.
Shirikisho la Mpira wa Miguu la Marekani (USSF) limemuombea hati hiyo Mbise kama mchezaji wa ridhaa ili ajiunge na timu ya Virginia Youth Soccer.
Klabu ya zamani ya Mbise aliyezaliwa Agosti 18, 1994 imetajwa kuwa Super Sport FC, na mechi ya mwisho kwenye timu hiyo alicheza Novemba 15 mwaka juzi.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanya mawasiliano na pande husika kabla ya kutoa hati hiyo kwa mchezaji huyo kama ilivyoombwa na shirikisho hilo la Marekani.
TWFA YATAKA ORODHA YA WAPIGA KURA
Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) chini ya Mwenyekiti wake Ombeni Zavala imewataka wanachama wa TWFA ambao ni mikoa ya Tanzania Bara kuwasilisha orodha ya wajumbe wao wa mkutano wa uchaguzi.
Wajumbe wenye sifa ya kuhudhuria Mkutano wa TWFA ni kutoka vyama vya mikoa ambavyo tayari vimefanya uchaguzi. Wajumbe hao ni Mwenyekiti, Katibu na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TWFA.
Mikoa ambayo imeshafanya uchaguzi mpaka sasa ni Iringa, Kigoma, Mwanza, Pwani na Tanga. Mikoa ambayo bado inahimizwa kufanya uchaguzi, na mwisho wa kutuma majina ya wajumbe kwa Mwenyekiti Zavala ni Oktoba 25 mwaka huu.
Mkoa ambao utakuwa haujafanya uchaguzi utakuwa umenyimwa haki ya kushiriki uchaguzi wa TWFA utakaofanyika Novemba 4 mwaka huu.
TASMA WAANZA MCHAKATO WA UCHAGUZI
Chama cha Madaktari wa Tiba ya Michezo Tanzania (TASMA) leo (Oktoba 19 mwaka huu) kimetangaza kuanza mchakato wa uchaguzi wa chama hicho uliopangwa kufanyika Novemba 28 mwaka huu.
Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TASMA, Dk. Francis Mchomvu, fomu kwa wanamichezo wanaotaka kugombea uongozi wa chama hicho zitaanza kutolewa Oktoba 21 mwaka huu.
Mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu hizo zinazopatikana ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni saa 10.00 alasiri ya Oktoba 26 mwaka huu. Ada ya fomu kwa nafasi nne za juu ni sh. 200,000 wakati kwa nafasi nyingine zilizobaki ni sh. 100,000. Kati ya Oktoba 27-31 mwaka huu Kamati ya Uchaguzi ya TASMA itapitia fomu na kutangaza majina ya waliojitokeza kuomba uongozi.
Nafasi zitakazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mhazini, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji.
Kipindi cha pingamizi kwa waombaji ni kuanzia Novemba 1-6 mwaka huu, na pingamizi zinatakiwa kuwasilishwa kwa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya TASMA kabla ya saa 10.00 alasiri ya Novemba 6 mwaka huu. Hakuna ada kwenye pingamizi.
Pingamizi zitajadiliwa na kufanyiwa uamuzi kati ya Novemba 7-9 mwaka huu. Usaili utafanyika kati ya Novemba 10-11 mwaka huu ambapo matokeo ya usaili huo vilevile yatatangazwa ili kutoa fursa kwa rufani ambazo zinatakiwa kukatwa kati ya Novemba 11-13 mwaka huu.
Rufani ambazo zinaambatana na ada y ash. 500,000 zinatakiwa kufikishwa kwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kabla ya saa 10.00 alasiri ya Novemba 13 mwaka huu.
YANGA, RUVU SHOOTING SASA KUCHEZA TAIFA KESHO
Mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya Yanga na Ruvu Shooting uliopangwa kuchezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) Uwanja wa Chamazi sasa umehamishiwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.15 jioni.
Mabadiliko hayo yamefanyika kutokana na maombi ya timu hizo mbili kutaka mechi ichezwe Uwanja wa Taifa kutokana na sababu mbalimbali ambazo zimeridhiwa na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikiwemo siku hiyo uwanja huo kutokuwa na mechi.
Viingilio katika mechi hiyo itakayokuwa chini ya mwamuzi Amon Paul kutoka Mara ni sh. 5,000 viti vya kijani na bluu, sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP B na C na sh. 20,000 kwa VIP A.
Pia Kamati ya Ligi imekataa ombi la timu ya Azam kutaka mechi zake za nyumbani za ligi hiyo zichezwe dhidi ya Simba na Yanga zichezwe Uwanja wa Chamazi kutokana na sababu za kiusalama.
Nayo Coastal Union itakuwa mwenyeji wa Mtibwa Sugar katika mechi nyingine ya ligi hiyo itakayochezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Mchezo huo namba 56 wa kukamilisha raundi ya nane utachezeshwa na mwamuzi Israel Nkongo atakayesaidiwa na Hamis Chang’walu na Omari Kambangwa, wote kutoka Dar es Salaam.
Ligi hiyo itaendelea tena Jumapili (Oktoba 21 mwaka huu) kwa mechi tatu. JKT Ruvu itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Chamazi, Mgambo Shooting itaikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wakati Tanzania Prisons na Toto Africans zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya.
Thursday, October 18, 2012
YANGA CHAGUENI NEMBO-VODACOM
Kampuni ya simu za mkononi Vodacom, ambao pia ni wadhamini wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, wamefikia muafaka na klabu ya Yanga juu ya kutotumia jezi zenye nembo nyekundu.
Vodacom imefikia hatua hiyo kufuatia Yanga kupeleka maombi yao ya kuomba kutotumia nembo hiyo nyekundu katika jezi zao.
Kufuatia maombi ya klabu ya Yanga kupitia kwa viongozi wake na baraza la wazee, vodacom imeona ni busara kuwasikiliza Yanga maombi yao na hivyo kuamua kuipa nafasi ya kuchagua nembo moja kati ya tatu.
Vodacom imetoa aina tatu za nembo na Yanga inapaswa kuchagua moja kati ya hizi nembo tatu.
TFF YAANZISHA USHIRIKIANO NA KFF
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya (FKF) yamefikia makubaliano ya kushirikiana katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuinua kiwango cha mpira wa miguu katika nchi hizo.
Akizungumza baada ya mkutano uliowakutanisha vinara wa mashirikisho hayo Dar es Salaam jana, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema wameamua kurejesha uhusiano huo uliokuwepo zamani baada ya kuwepo utulivu katika uendeshaji mpira wa miguu nchini Kenya.
Amesema maeneo ya ushirikiano ambayo wameagiza yafanyiwe kazi na sekretarieti za pande zote (TFF na KFF) ili baadaye yaingizwe katika Hati ya Makubaliano (MoU) ni mafunzo, waamuzi, mechi za timu za Taifa za wakubwa, vijana na wanawake, na Ligi Kuu.
Rais Tenga pia amesema wameamua kuwepo ziara za mafunzo (study tours) katika maeneo mbalimbali ambapo kwa Kenya wao Ligi Kuu yao iliingia katika mfumo wa kampuni mapema, hivyo itakuwa fursa nzuri kwa Bodi ya Ligi Kuu ambayo iko kwenye mchakato wa kuanzishwa kupata uzoefu kwa wenzao wa Kenya.
Naye Rais wa FKF, Sam Nyamweya aliyefuatana na Makamu wake wa Rais, Robert Asembo amesema ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya ni wa kihistoria, hivyo wameamua kuuanzisha upya kwa faida ya nchi hizo.
Amesema hivi karibuni FKF ilichukua waamuzi kutoka Tanzania waliochezesha mechi ya kirafiki kati ya Kenya (Harambee Stars) na Afrika Kusini (Bafana Bafana), hivyo wameamua kubadilishana waamuzi kwa lengo la kuwaongezea uzoefu.
“Waamuzi wa Tanzania walichezesha vizuri mechi ile. Unajua kwetu kuna upinzani mkubwa katika klabu kama AFC Leopards na Gor Mahia, ukipanga refa utasikia wengine wanalalamika, mara huyo ni Mjaluo. Hata akichezesha vizuri bado watalalamika tu kutokana na upinzani uliopo katika klabu hizo,” amesema.
Rais Nyamweya ameongeza kuwa ili kuondoa malalamiko katika mechi za aina hiyo wanaweza kuchukua waamuzi kutoka Tanzania, na vilevile waamuzi kutoka Kenya wakachezesha mechi za aina hiyo nchini Tanzania.
Amesema vilevile wamepanga kuangalia uwezekano wa kuwa na mechi za kuandaa timu kabla ya kuanza Ligi Kuu za nchi hizo ambapo washindi watatu au wanne wa kwanza katika ligi hizo kushindana.
Kwa upande wa mafunzo, wamekubaliana kuwa kwa vile kila nchi ina wakufunzi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na la Afrika (CAF) watawatumia kuandaa mafunzo ya mara kwa mara kwa waamuzi, makocha, madaktari wa tiba ya michezo na viongozi badala ya kusubiri mafunzo ya aina hiyo kutoka kwa mashirikisho hayo ya kimataifa.
SIMBA, KAGERA SUGAR ZAINGIZA MIL 58/-
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Kagera Sugar lililochezwa jana (Oktoba 17 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 limeingiza sh. 58,505,000.
Watazamaji 9,842 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyochezwa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000, na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 11,013,785.54 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,924,491.53.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni posho ya msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 250,000, waamuzi sh. 440,000, mtathimini wa waamuzi sh. 254,000, mwamuzi wa akiba sh. 70,000, usafi na ulinzi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (stadium technical support) sh. 2,000,000.
Umeme sh. 300,000, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, ulinzi wa mechi sh. 3,500,000 wakati tiketi ni sh. 3,183,890. Gharama za mchezo sh. 3,671,261.85, uwanja sh. 3,671,261.85, Kamati ya Ligi sh. 3,671,261.85, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,202,757.11 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,468,504.74.
YONDAN: ACHENI KUNICHONGANISHA NA BOBAN
KITENDO cha kiungo Haruna Moshi 'Boban' wa Simba kumchezea rafu mbaya beki, Kelvin Yondan wa Yanga kilipokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki wa soka nchini, hasa wa klabu hizo mbili kongwe na zenye mashabiki lukuki.
Tukio hilo lilitokea Oktoba 3 mwaka huu wakati Simba ilipomenyana na Yanga katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika mechi hiyo, timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1.
Wapo waliomuona Boban kuwa alifanya kitendo kile kwa makusudi kwa lengo la kupunguza makali ya safu ya ulinzi ya Yanga, iliyokuwa ikiongozwa na Yondan, lakini wengine walilitafsiri kuwa ni tukio la kawaida katika soka.
Siku chache baada ya mechi hiyo, Boban alijitokeza hadharani na kumuomba radhi Yondan pamoja na mashabiki wa Yanga kwa madai kuwa, tukio hilo lilikuwa la bahati mbaya na kwamba hakuwa amedhamiria kumuumiza mchezaji mwenzake huyo wa zamani wa Simba.
Boban alikwenda mbali zaidi kwa kudai kuwa, yeye na Yondan walikuwa marafiki wakubwa walipokuwa pamoja Simba na kwenye kikosi cha timu ya Taifa, Taifa Stars, hivyo isingekuwa rahisi kudhamiria kumvunja.
Kufuatia rafu hiyo, Yondan alilazimika kukaa nje ya uwanja kwa wiki mbili, akiuguza mguu wake, ambao ulivunjika mfupa mdogo. Tayari beki huyo ameshaanza mazoezi na wenzake na anatarajiwa kurejea uwanjani hivi karibuni.
Tukio hilo pia lilisababisha mwamuzi Mathew Akrama kutoka Mwanza, aliyechezesha mechi hiyo, aondolewe kwenye orodha ya waamuzi kwa kosa la kuvurunda na pia kushindwa kumuonyesha kadi nyekundu Boban kutokana na kutenda kosa hilo.
Akihojiwa na Burudani mjini Dar es Salaam wiki hii, Yondan alisema anaamini Boban hakuwa amekusudia kumvunja mguu kwa makusudi bali ni tukio la bahati mbaya na kawaida katika soka.
Yondan alisema hana kinyongo na Boban kutokana na rafu hiyo na kusisitiza kuwa, ni rafiki yake wa karibu na amekuwa akimtembelea mara kadhaa ikiwa ni pamoja na kumuomba radhi.
"Nawaomba mashabiki wa Yanga watulie na kuniombea dua nirudi uwanjani mapema na nikiwa na afya njema,"alisema Boban, ambaye aliwashukuru viongozi wa Yanga kwa kusimamia matibabu yake kwa umakini mkubwa.
Kwa mujibu wa Yondan, Boban alimfuata nyumbani kwake siku chache baada ya mchezo ule na kumuomba radhi kutokana na tukio lile na kusisitiza kuwa, uamuzi wake huo ulimfanya amuone muungwana.
"Binafsi nilimuelewa na kumsamehe kwa vile kitendo alichokifanya ni cha kiungwana na kiuanamichezo. Nawaomba mashabiki wasitumie tukio lile kunichonganisha na Boban. Wasiwe na kinyongo naye chochote,"alisisitiza.
Alipoulizwa kuhusu uamuzi wake wa kuihama Simba na kujiunga na Yanga, Yondan alikiri kwamba ulikuwa mgumu kwa vile alikumbana na vipingamizi vingi kutoka kwa viongozi na wanachama wa Simba.
Yondan alisema binafsi aliamua kujiunga na Yanga kutokana na ofa nzuri aliyopewa na viongozi wa klabu hiyo na kuongeza kuwa, lengo la mwanasoka yeyote siku zote huwa ni kukitumia kipaji chake kupata pesa za kuweza kuyaendesha vizuri maisha yake.
"Viongozi wa Yanga wamenipa mkataba mzuri, ambao ndani yake kuna vitu vingi, ambavyo kwa asilimia kubwa vimetimizwa. Kwa sasa nina furaha kubwa ya kuichezea Yanga," alisema beki huyo kisiki.
Yondan amewashukuru viongozi, wanachama na wachezaji wenzake kwa kumpa ushirikiano mzuri tangu alipojiunga na klabu hiyo na kuongeza kuwa, lengo lake kubwa ni kusaidia ili iweze kufanya vizuri katika michuano mbali mbali.
Beki huyo alikiri kuwa, changamoto kubwa inayomkabili kwa sasa ni kupigania namba kwenye kikosi cha kwanza kutokana na ukweli kwamba, timu hiyo inaundwa na wachezaji wengi wazuri katika idara zote.
Yondan pia aliwashukuru viongozi na wanachama wa Simba kwa kumpa ushirikiano mkubwa alipokuwa akiichezea timu hiyo na kusisitiza kuwa, kuondoka kwake kulilenga kutafuta malisho mazuri zaidi.
"Unajua soka ni mchezo wa muda mfupi, ukifanya makosa unaweza kujiharibia kila kitu, hivyo mchezaji unapaswa kuwa makini katika kujenga maisha yako ya baadaye,"alisema.
Yondan alisema ameondoka Simba akiwa hana kinyongo na kiongozi ama mchezaji yeyote na kwamba hata anapokutana nao, wamekuwa wakisalimiana na kuzungumza vizuri.
Beki huyo kisiki wa Yanga alisema, katika muda wote ambao amekuwa akicheza soka, amekutana na changamoto nyingi na kubaini kuwepo kwa vitu vingi ndani ya soka, lakini ni mapema kuvizungumza kwa sasa.
Alisisitiza kuwa, jambo la muhimu ni kwa viongozi wa klabu za soka kuwatimizia wachezaji wao yale yanayokuwemo kwenye mikataba kati yao na kuacha kutoa ahadi zisizotekelezeka.
Alisema matatizo mengi yanayotokea sasa kati ya wachezaji na viongozi wa klabu, yanatokana na viongozi kupenda kutoa ahadi kwa wachezaji na kuwatelekeza wanapopatwa na matatizo.
Ametoa ushauri kwa viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutilia mkazo ufuatiliaji wa vipaji vya vijana na kuwaendeleza kwa kuwekeza zaidi kwenye soka la vijana na kuziimarisha timu za taifa za vijana wa umri mbali mbali.
MOSHA, SAUKO KUONGEZA NGUVU YANGA
UONGOZI wa klabu ya Yanga umepanga kuwaongeza makamu mwenyekiti wa zamani wa klabu hiyo, Davis Mosha na Abdul Sauko kwenye kamati ya mashindano kwa ajili ya kuongeza nguvu.
Habari zilizopatikana jana kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa, uamuzi wa kuwaongeza Mosha na Sauko kwenye kamati hiyo,ulifikiwa hivi karibuni kwenye kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo.
Katika kikao hicho, wajumbe waliafiki kwa kauli moja kuongezwa kwa Mosha na Sauko kwenye kamati hiyo kutokana na uzoefu wao katika uongozi wa soka na kusimamia timu.
Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ameieleza Burudani kuwa, kamati hiyo kwa sasa imepwaya kutokana na kutokuwa na wapiganaji wenye uwezo wa kupambana na timu pinzani.
"Tumeona wajumbe wengi waliopo sasa kwenye kamati hiyo hawafahamu vyema fitina za soka kama walivyo Mosha na Sauko,"alisema mjumbe huyo.
Kwa mujibu wa mjumbe huyo, Mwenyekiti wa Yanga, Yussuf Manji anatarajia kuwatangaza rasmi wajumbe hao wapya baada ya kurejea nchini kutoka Makka, ambako amekwenda kwa ajili ya ibada ya hija.
Katika hatua nyingine, kuchelewa kurejea nchini kwa mshambuliaji, Hamisi Kiiza wa Yanga kumezusha hali ya wasiwasi katika benchi la ufundi la timu hiyo.
Kiiza alikwenda Uganda kwa ajili ya kuichezea timu hiyo katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika za mwaka 2013 zitakazofanyika Afrika Kusini.
Katika mechi hiyo dhidi ya Zambia iliyopigwa mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Kampala, Uganda ilitolewa kwa mikwaju ya penalti baada ya matokeo ya jumla kuwa sare ya bao 1-1.
Habari kutoka katika benchi la ufundi la Yanga zilieleza jana kuwa, Kiiza ilikuwa arejee nchini juzi, lakini alishindwa kutokana
na kuuguliwa na mtoto wake.
Kwa mujibu wa habari hizo, mchezaji huyo sasa anatarajiwa kurejea nchini leo kwa ajili ya kujiandaa kwa mechi ya ligi kuu dhidi ya Ruvu Shooting, itakayopigwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
MAJAMBAZI WALIONIPORA NI MASHABIKI WANGU-JULIET
ACCRA, Ghana
MCHEZA filamu Juliet Ibrahim wa Ghana amesema majambazi
yaliyompora vitu vyenye thamani mbali mbali nyumbani kwake, ni
mashabiki wake wakubwa.
Juliet amewaelezea majambazi hao kuwa ni mashabiki wake
kutokana na kutomdhuru yeye na familia yake.
Baadhi ya vyombo vya habari viliripoti hivi karibuni kuwa, Juliet
alikutwa na mkasa huo kwenye uwanja wa ndege wa Accra wakati
alipokuwa akirejea kutoka safarini Marekani.
Hata hivyo, Juliet alisema si kweli kwamba tukio hilo lilitokea
uwanja wa ndege. Alisema majambazi hao walimpora baada ya
kufika nyumbani kwake.
Alisema katika tukio hilo, majambazi hao walipora simu zao za
mkononi na pesa taslim, lakini hakuwa tayari kutaja thamani yake.
"Napenda kila mmoja afahamu kwamba, nipo katika hali nzuri mimi
na familia yangu na tukio la kuporwa lilitokea nyumbani, si uwanja
wa ndege,"alisema.
Kwa mujibu wa Juliet, tukio hilo lilitokea saa tatu usiku wakati
umeme ulipokuwa umekatika katika maeneo mengi ya Jiji la Accra.
"Kama kungekuwa na mwangaza, tungeweza kuwaona majambazi
hao walipoegesha gari lao jeusi. Nadhani katika kipindi hiki, kuna
matukio mengi yatakayotokea kwa sababu ya tatizo la kukatika kwa
umeme nchi nzima,"aliongeza.
Aliongeza kuwa, anachoshukuru ni kwamba yeye na familia yake
hawakupata madhara yoyote wakati wa tukio hilo.
"Natumaini majambazi hawa watakuwa wakisoma ujumbe huu.
Napenda kusema asante kwao kwa kutimiza maneno yao ya
kutoidhuru familia yangu. Ni mashabiki wazuri kwangu,"alisema
Juliet.
MIMBA YA INI EDO YAHARIBIKA
LAGOS, Nigeria
UTATA umezuka kuhusu uja uzito wa mcheza filamu nyota wa kike
wa Nigeria, Ini Edo baada ya kuripotiwa kuwa mimba yake
imeharibika.
Gazeti la Encomium la Nigeria liliripoti wiki hii kuwa, Ini amekuwa
akionekana katika hali ya kawaida, licha ya kuwepo na taarifa
kwamba alikuwa akikaribia kujifungua.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, katika hafla mbali mbali ambazo Ini
alihudhuria siku za hivi karibuni, tumbo lake limekuwa likionekana
la kawaida, hali inayozua maswali mengi.
Katika moja ya picha alizopiga hivi karibuni, Ini alionekana akiwa
amefunga mkanda mkubwa kwenye tumbo lake na kusababisha
watu kujiuliza maswali mengi.
"Ini amepoteza uja uzito wa mumewe, Philip Ehiagwina," liliripoti
gazeti hilo.
Gazeti hilo liliripoti kuwa, miezi michache iliyopita, Ini alithibitisha
kuwa na uja uzito wa miezi minane na kwamba alikuwa akikaribia
kujifungua.
"Watu walio karibu na Ini Edo wamesema, katika sherehe ya
kuzaliwa ya mwigizaji mwenzake, Stephanie Linus, Ini alionekana
kuwa katika hali ya kawaida bila ya kuwa na dalili za uja uzito,"
limeeleza gazeti hilo.
"Kama mimba yake haikuharibika, hivi sasa angekuwa kitandani
akikaribia kujifungua," lilieleza gazeti hilo.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, Oktoba 8 mwaka huu, mwandishi wake
aliwasiliana na Ini kwa simu na kuzungumza na msaidizi wake,
aliyetambulika kwa jina la Edward, ambaye alisema alikuwa amelala
wakati huo.
"Sifahamu lolote kuhusu mimba yake kuharibika," gazeti hilo
lilimkariri msaidizi huyo wa Ini akisema.
"Inawezekana atakapoamka, atazungumzia suala hilo. Lakini
sifahamu lolote kuhusu taarifa hizo," alisemamsaidizi huyo wa Ini.
Gazeti hilo liliendelea kuripoti kuwa, liliwasiliana na Ini mara kadhaa
kwa njia ya simuna ujumbe wa maandishi, lakini hakuwa akipokea
wala kuzijibu.
Ujumbe uliotumwa na gazeti hilo kwa Ini ulisomeka hivi: "Tulikupigia
simu, lakini Edward alisema ulikuwa umelala.
Kuna taarifa hapa kwamba, mimba yako imeharibika na
tungependa kupata ukweli kutoka kwako kabla ya kuchapisha
habari hizi."
DIAMOND AFURAHIA KUITWA MFALME WA BONGO FLEVA
MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul ameelezewa kuwa ndiye Mfalme wa Bongo Fleva kwa sasa hapa nchini.
Naseeb, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la Diamond, amepewa hadhi hiyo na mtandao wa MSN Africa.
Mbali na Diamond, mtandao huo pia umemtaja Judith Wambura Lady JayDee kuwa ndiye malkia wa muziki wa miondoko hiyo hapa nchini.
Kwa mujibu wa MSN Africa, Diamond na JayDee wanastahili hadhi hiyo kutokana na mafanikio mbali mbali waliyoyapata kimuziki.
Diamond ameeleza kupitia tovuti yake wiki hii kuwa, amepata furaha kubwa kutokana na hadhi aliyopewa na mtandao huo.
"Kiukweli, nimejisikia furaha kubwa kuandikwa katika mtandao mkubwa kama huu juu ya kazi zangu za muziki ninazozifanya," ameeleza Diamond katika sehemu ya taarifa yake aliyoitoa kwenye mtandao wake.
"Tena kubwa zaidi ni kupewa heshima hii ya kuwa Mfalme wa Bongo Fleva. Kiukweli imenipa matumaini sana ingawa nafsi yangu inaniambia bado sistahili kuitwa jina hilo kwani nina safari ndefu sana," aliongeza msanii huyo.
Diamond amewashukuru mashabiki wa muziki nchini kwa kuendelea kumuunga mkono kutokana na kazi zake na kuufanya muziki wa bongo fleva kuanza kupata umaarufu barani Afrika.
Ameishukuru familia yake, hasa mama yake mzazi na menejimenti inayosimamia kazi zake kwa kumuunga mkono muda wote wa kazi yake.
Diamond ni miongoni mwa wasanii, ambao wamekuwa wakitwaa mara kwa mara tuzo za muziki za Kilimanjaro kutokana na muziki wake kukubalika na mashabiki wengi, ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.
Msanii huyo ameelezwa kuwa, ndiye anayeongoza kwa mapato yatokanayo na muziki na pia kualikwa katika nchi mbali mbali kufanya maonyesho.
Katika hatua nyingine, Diamond amewatahadharisha mashabiki wake kuhusu baadhi ya watu wanaotumia anwani yake ya facebook na twitter kuomba misaada ya pesa.
Diamond ameeleza kupitia tovuti yake kuwa, watu hao pia wamekuwa wakitumia akaunti zake kutoa maneno machafu kwa mashabiki wake.
"Nimevumilia sana hii tabia, lakini naona kama uzalendo umenishinda. Mara kwa mara nimekuwa nikipokea malalamiko kutoka kwa wadau wangu, mbali mbali kwamba nawajibu vibaya kwenye akaunti yangu ya facebook, kutoa maneno machafu na kuweka picha chafu,"alisema.
"Kibaya zaidi, watu hawa wamekuwa wakiomba pesa kwa njia ya Western Union, M-Pesa, Tigo Pesa na nyinginezo. Kiukweli jambo hili limekuwa likinisikitisha sana,"aliongeza.
Diamond amesema akaunti hiyo yenye jina la Diamond Platnums Swaqq ni feki kwa sababu siyo ya kwake, ni ya mtu anayetumia jina na picha zake kuwachezea akili mashabiki wake.
Wakati huo huo, Diamond ametoa mwito kwa watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya kitalii vilivyopo nchini.
Diamond alitoa mwito huo wiki iliyopita baada ya kutembelea Hifadhi ya Ngorongoro iliyopo mkoani Arusha.
Akizungumza baada ya ziara yake hiyo, Diamond alisema kamwe katika maisha yake hakuwahi kufikiria iwapo Tanzania inavyo vivutio vizuri vya kitalii kama Hifadhi ya Ngorongoro.
Alisema alikuwa akiviona vivutio hivyo kupitia vipindi mbali mbali vya televisheni, lakini baada ya kuvishuhudia kwa macho yake, anatamani kuvitembelea mara kwa mara.
SIMBA YAVUTWA SHARUBU
SIMBA jana ililazimishwa kutoka sare ya mabao 2-2 na Kagera Sugar katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Licha ya kulazimishwa sare, Simba bado inaendelea kuongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 18 baada ya kucheza mechi nane, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 17, JKT Oljoro yenye pointi 13 na Kagera Sugar yenye pointi 12.
Simba itabidi ijilaumu kwa kushindwa kutoka uwanjani na ushindi kwani iliweza kuongoza mabao 2-0 hadi dakika ya 61 wakati Kagera ilipopata bao na hatimaye kusawazisha.
Kagera ililianza pambano hilo kwa kasi na kupata kona dakika ya kwanza, lakini haikuwa na madhara yoyote kwenye lango la Simba.
Simba ilipata nafasi nzuri ya kufunga bao dakika ya saba wakati Felix Sunzu alipojitwisha kwa kichwa mpira wa krosi uliopigwa na Nassoro Masoud kutoka pembeni ya uwanja, lakini uliokolewa na kipa Andrew Ntalla wa Kagera.
Sunzu alisahihisha makosa dakika ya nane baada ya kuifungia Simba bao kwa kichwa, kufuatia krosi maridhawa iliyopigwa na Mrisho Ngasa.
Daudi Jumanne nusura aipatie bao Kagera dakika ya 25 baada ya kumtoka Amri Kiemba wa Simba na kufumua shuti kali, lakini lilitoka pembeni ya lango.
Haruna Moshi aliikosesha Simba nafasi nzuri ya kufunga bao dakika ya 32 alipobaki ana kwa ana na kipa Ntalla, baada ya kupokea pasi kutoka kwa Emmanuel Okwi, lakini shuti lake lilitoka nje. Timu hizo zilikwenda mapumziko Simba ikiwa mbele kwa bao 1-0.
Kagera ilipata bao la kwanza kupitia kwa Themi Felix kabla ya Salum Kanoni kuisawazishia kwa njia ya penalti baada ya beki Nassoro Masoud kumwangusha Paul Ngwai ndani ya eneo la hatari.
SIMBA: Juma Kaseja, Nassoro Masoud, Amir Maftah, Paschal Ochieng, Juma Nyoso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Haruna Moshi, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Mrisho Ngasa.
KAGERA SUGAR: Andrew Ntalla, Salum Kanoni, Martin Muganyizi, Amandus Nesta, Benjamin Effe, Malagesi Mwangwa, Daudi Jumanne, George Kavilla, Shija Mkina, Enyima Darlington, Wilfred Ammeh.
AHMED AMASHA 'MATHEMATICIAN': SIVUTIWI NA KIWANGO CHA TAIFA STARS
L Aziponda Simba na Yanga kwa kupapatikia wachezaji wa kigeni
L Ataka klabu za ligi kuu ziwekeze zaidi kwenye soka ya vijana
L Bado alikumbuka jinamizi la Yussuf Ambwene wa CDA
JINA la Ahmed Amasha si geni miongoni mwa mashabiki wa soka nchini. Ni mmoja wa wachezaji waliojipatia sifa kubwa kutokana na staili ya uchezaji wake kiasi cha kupachikwa jina la Mathematician.
Amasha alianza kujipatia umaarufu mwaka 1980 baada ya kujiunga na Tumbaku ya Iringa kabla ya kuhamishiwa Tumbaku ya Morogoro, iliyokuwa ikishiriki michuano ya ligi daraja la kwanza.
Mwaka huo huo, Amasha alichaguliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, Taifa Stars, ambacho kilishiriki kwa mara ya kwanza kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizofanyika nchini Nigeria.
Katika kikosi hicho, Amasha alikuwa akicheza nafasi ya kiungo mkabaji, lakini baada ya kuumia kwa beki wa kushoto, Mohamed Kajole, Makocha Slowmir Work kutoka Poland na Joel Bendera waliamua kumuhamishia nafasi hiyo.
Amasha alicheza mechi zote tatu, ambazo Taifa Stars ilicheza katika fainali hizo. Katika mechi ya kwanza, Taifa Stars ilichapwa mabao 3-1 na wenyeji Nigeria, ikacharazwa mabao 2-1 na Misri kabla ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Ivory Coast.
Wachezaji wengine waliokuwa wakiunda kikosi cha Taifa Stars wakati huo ni Athumani Mambosasa, Mohamed Rishard Adolph, Kajole. Jella Mtagwa, Leodegar Tenga, Hussein Ngulungu, Mohamed Salim, Omar Hussein, Peter Tino, Leopald Tasso Mukebezi na wengineo.
Baada ya kurejea kutoka Nigeria, Amasha alijiunga na klabu ya Yanga na kuichezea kwa miaka sita, ikiwa ni pamoja na kuiwezesha kutwaa ubingwa wa ligi kuu mara tatu.
Katika kikosi hicho cha Yanga, Amasha alicheza pamoja na Hamisi Kinye, Yussuf Bana, Athumani Chama,Isihaka Hassan, Allan Shomari, Charles Boniface, Juma Mkambi, Abeid Mziba, Makumbi Juma, Saleh Hija,Hussein Iddi, Juma Kampala, Joseph Fungo na wengineo.
Amasha, ambaye aliwahi kuchaguliwa kuwa mwanasoka bora wa Tanzania mwaka 1984, aliichezea Yanga katika michuano ya ligi, klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati pamoja na klabu bingwa Afrika, ambapo timu hiyo kongwe ilikuwa ikitolewa hatua za awali.
Mwaka 1986, Amasha aliamua kuondoka nchini na kwenda Arabuni, ambako alijiunga na timu ya Fanja, iliyokuwa ikiundwa na wachezaji wengi kutoka Afrika, wakiwemo watanzania.
Wachezaji kutoka Tanzania aliocheza nao kwenye kikosi hicho ni pamoja na Twalib Hilali, Hilal Hemed na Abdulwakati Juma kutoka Zanzibar.
Alidumu Fanja kwa miaka minne, ikiwa ni pamoja na kuiwezesha kutwaa ubingwa wa nchi hiyo mara kadhaa pamoja na kombe la Mfalme.
Baadaye alijiunga na klabu ya Dhofar, aliyoichezea kwa miaka minne kabla ya kuhamia Saeeb, ambayo aliichezea kwa miaka mitatu na kutwaa nayo mataji kadhaa.
Kwa sasa, Amasha ni kocha msaidizi katika klabu ya Saeeb. Aliamua kuchukua mafunzo ya ukocha na kupata leseni daraja C na B baada ya kustaafu kucheza soka.
Moja ya matukio, ambayo yataendelea kubaki kwenye kumbukumbu ya Amasha ni lile la kuvunjika mguu beki Yussuf Ambwene wa CDA katika mechi ya ligi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ambwene alivunjika mguu baada ya kugongana na Amasha wakati wakigombea mpira na jeraha hilo lilisababisha alazwe hospitali ya Muhimbili kwa wiki kadhaa na hatimaye kulazimika kuachana kabisa na soka.
Akizungumza na Burudani mjini Dar es Salaam wiki hii, Amasha alisema hakuwa amedhamiria kumuumiza Ambwene, bali waligongana kwa bahati mbaya.
Amasha alikiri kuwa, tukio hilo lilimsababishia matatizo makubwa ikiwa ni pamoja na baadhi ya mashabiki kudhani alidhamiria kumuumiza mchezaji huyo kwa makusudi.
“Katika soka, jambo kama hilo kutokea ni la kawaida, lakini maneno ya watu huwezi kuyazuia. Lilitokea kwa bahati mbaya ndiyo sababu nilikuwa nikimtembelea mara kwa mara alipolazwa hospitali na hata alipokuwa Dodoma,”alisema.
Akizungumzia kiwango cha soka nchini, Amasha alisema kipo juu kwa klabu za Simba na Yanga, lakini ni cha chini kwa klabu zingine, hasa za mikoani, tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Alisema alibahatika kushuhudia mechi ya ligi kuu ya watani wa jadi, Simba na Yanga iliyochezwa Oktoba 3 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuvutiwa na viwango vya baadhi ya wachezaji.
Aliwataja wachezaji waliomvutia kuwa ni safu ya ulinzi ya Simba, iliyokuwa ikiundwa na Nassoro Masoud Cholo, Paul Ngelema, Shomari Kapombe, Juma Nyoso na Jonas Mkude.
Kwa upande wa Yanga, aliwataja wachezaji waliomvutia kuwa ni Athumani Iddi Chuji na nyota wa kigeni, Haruna Niyonzima na Didier Kavumbagu.
Amasha alisema pia kuwa, alipata nafasi ya kushuhudia mechi ya fainali ya Kombe la Kagame kati ya Yanga na Azam, ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 na kutwaa ubingwa.
Kwa mujibu wa Amasha, katika mechi hiyo alivutiwa na viwango vya mshambuliaji John Bocco na kiungo Salum Abubakar, ambao alisema wana uwezo wa kucheza soka ya kimataifa barani Ulaya.
Amasha alilaumu tabia ya klabu kubwa za soka nchini kuwapa vipau mbele katika usajili wachezaji wa kigeni na kuwaacha wanasoka wazalendo wenye vipaji.
Alisema havutiwi na staili hiyo ya usajili kwa sababu baadhi ya wachezaji wa kigeni waliosajiliwa na Simba na Yanga, uwezo wao ni wa chini ikilinganishwa na wanasoka wazalendo.
“Enzi zetu, soka ilitiliwa umuhimu sana kuanzia shule ya sekondari. Huko ndiko tulikotokea wachezaji wengi wa zamani, ambao baadhi yetu tulichezea Simba, Yanga na Taifa Stars,”alisema.
Aliwataja baadhi ya wachezaji aliocheza nao katika michezo ya shule za sekondari nchini kuwa ni pamoja na George Kulagwa, Nico Njohole, Abbas Kuka, Rahim Rumelezi, Peter Mhina, Salim Omar, Charles Mngodo na wengineo.
Amasha alisema hafurahishwi na kiwango kinachoonyeshwa na Taifa Stars katika michuano ya kimataifa kutokana na makocha wanaoteuliwa kuinoa timu hiyo kubadili wachezaji mara kwa mara.
Alisema itakuwa vigumu kwa Taifa Stars kupata mafanikio katika michuano ya kimataifa,iwapo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) halitawekeza katika soka ya vijana na kuziimarisha timu za vijana wa umri mbali mbali.
Aliipongeza klabu ya Simba kwa kuwa na timu nzuri za vijana, ikiwemo ya vijana wa chini ya miaka 20, ambayo ilifanikiwa kutwaa Kombe la Benki ABC hivi karibuni baada ya kuzifunga timu ngumu za Azam na Mtibwa Sugar.
Alisema ni vyema klabu zingine za ligi kuu kuiga mfano huo ili ziweze kuwa na timu bora hapo baadaye badala ya kutegemea wachezaji wa kigeni.
Amasha alisema inafurahisha kuona kuwa, mashabiki wa soka nchini wana mwamko mkubwa wa kuhudhuria mechi za ligi na kimataifa, lakini timu zao hazifiki mbali.
Mkongwe huyo alisema iwapo pesa zilizopo sasa katika soka zingekuwepo enzi zao, Taifa Stars iliyocheza fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 1980, ingekuwa na uwezo wa kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Amasha alisema pesa zinazotumika sasa katika usajili wa wachezaji wa kigeni na kuwalipa mishahara zingekuwa zikitumika kuimarisha timu za vijana, Tanzania ingekuwa imepiga hatua kubwa kimaendeleo.
Alisema wachezaji waliokuwa wakiunda kikosi hicho walikuwa na vipaji vya aina yake na uwezo mkubwa wa kucheza soka na kuonyesha maajabu kuliko waliopo hivi sasa.
Mwanasoka huyo wa zamani alisema pia kuwa, wanasoka wa Tanzania wanashindwa kupata soko nje kutokana na vyombo vya habari nchini kuwapa kipaumbele wanasoka wa kigeni.
“Kila ukisoma magazeti na kutazama televisheni, utasikia habari za akina Okwi na Niyonzima. Hakuna wachezaji wazalendo wanaosifiwa na kama wapo ni wachache. Utaratibu huu hauwezi kuwasaidia kuwatangaza kimataifa,”alisema.
Mwanasoka huyo mkongwe anayeishi na kufanyakazi ya ukocha Arabuni ametoa mwito kwa vyama vya soka vya wilaya,mikoa na TFF kuchagua viongozi wenye sifa na kuongoza mchezo huo.
“Ni vyema kuwepo na mabadiliko katika uongozi wa soka. Tusichagua ilimradi viongozi. Tuchague watu waliowahi kucheza soka na wanaofahamu ABC ya mchezo huo,”alisema Amasha.
“Haiwezekani kwa mtu, ambaye hajawahi kucheza soka kupewa uongozi. Mtu wa aina hii hawezi kuleta mabadiliko yoyote zaidi ya kuitumia nafasi hiyo kwa maslahi yake binafsi,”aliongeza.
Amasha ametoa mwito kwa wanasoka wa Tanzania kuacha kuweka pesa mbele zaidi kuliko mchezo wenyewe. Alisema enzi zao, walikuwa wakiweka mbele zaidi uzalendo ndio sababu waliweza kucheza soka kwa miaka mingi.
Tuesday, October 16, 2012
SIMBA, KAGERA SUGAR KAZI IPO KESHO
Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi nane kesho (Oktoba 17 mwaka huu) kwa mechi tano huku vinara wa ligi hiyo Simba wakiialika Kagera Sugar kutoka mkoani Kagera kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mechi hiyo namba 52 itachezeshwa na mwamuzi Ronald Swai kutoka Arusha wakati waamuzi wasaidizi ni Julius Kasitu na Methusela Musebula, wote kutoka Shinyanga. Mwamuzi wa akiba ni Ephrony Ndisa wa Dar es Salaam huku mtathimini wa waamuzi akiwa Charles Mchau kutoka Moshi.
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Tanzania Prisons inayofundishwa na Jumanne Chale na Azam iliyo chini ya kocha Boris Bunjak kutoka Serbia. Nayo Polisi Morogoro iliyopanda msimu huu itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Jamhuri.
Mgambo Shooting ambayo imepata ushindi mara mbili mfululizo itakuwa nyumbani Uwanja wa Mkwakwani, jijini Tanga ikiikaribisha Toto Africans katika mechi itakayochezeshwa na Geofrey Tumaini wa Dar es Salaam.
Oljoro JKT inayonolewa na Mbwana Makata itakuwa nyumbani Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha dhidi ya African Lyon.
LIGI DARAJA LA KWANZA KUANZA OKTOBA 24
Michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ya Tanzania Bara inaanza rasmi Oktoba 24 mwaka huu kwa timu 18 kati ya 24 kujitupa kwenye viwanja tisa tofauti katika ligi hiyo inayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Mechi za raundi ya kwanza za kundi A zitakazochezwa Oktoba 24 mwaka huu ni Burkina Faso dhidi ya Mbeya City (Jamhuri, Morogoro), Mlale JKT na Small Kids (Majimaji, Songea) na Kurugenzi Mufindi
dhidi ya Majimaji (Uwanja wa Wambi, Mufindi mkoani Iringa).
Mkamba Rangers na Polisi Iringa zitakamilisha raundi ya kwanza kwa kundi hilo Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Mechi za raundi ya pili kwa kundi hilo zitachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwa Polisi Iringa vs Mbeya City (Samora, Iringa), Majimaji vs Small Kids (Majimaji, Songea), Burkina Faso vs Mkamba Rangers (Jamhuri, Morogoro) na Kurugenzi Mufindi vs Mlale JKT (Wambi, Mufindi).
Raundi ya tatu ni Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Mbeya City vs Mlale JKT (Sokoine, Mbeya), Small Kids vs Mkamba Rangers (Nelson Mandela, Sumbawanga), Majimaji vs Burkina Faso (Majimaji, Songea) na Polisi Iringa vs Kurugenzi Mufindi (Samora, Iringa).
Kundi B Oktoba 24 mwaka huu ni Ndanda vs Transit Camp (Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Moro United (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 25 mwaka huu ni Green Warriors vs Tessema (Mabatini, Pwani) na Polisi Dar es Salaam vs Ashanti United (Chamazi, Dar es Salaam).
Raundi ya pili kwa kundi hilo ni Oktoba 27 mwaka huu Ndanda vs Green Warriors (Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Tessema (Mabatini, Pwani) wakati Oktoba 28 mwaka huu ni Ashanti United vs Transit Camp (Mabatini, Pwani) na Oktoba 29 mwaka huu ni Moro United vs Polisi Dar es Salaam (Chamazi, Dar es Salaam).
Novemba 1 mwaka huu ni Green Warriors vs Ashanti United (Mabatini, Pwani), Novemba 2 mwaka huu ni Polisi Dar es Salaam vs Villa Squad (Chamazi, Dar es Salaam), Novemba 4 mwaka huu ni Tessema vs Ndanda (Chamazi, Dar es Salaam) na Transit Camp vs Moro United (Mabatini, Pwani).
Kundi C ni Oktoba 24 mwaka huu Kanembwa FC vs Polisi Dodoma (Lake Tanganyika, Kigoma), Mwadui vs Morani (Kambarage, Shinyanga), Pamba vs Polisi Mara (Kirumba, Mwanza) na Rhino Rangers vs Polisi Tabora (Ali Hassan Mwinyi, Tabora).
Raundi ya pili ni Oktoba 27 mwaka huu; Polisi Tabora vs Polisi Dodoma (Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mwadui vs Polisi Mara (Kambarage, Shinyanga), Kanembwa FC vs Morani (Lake Tanganyika, Kigoma) na Pamba vs Rhino Rangers (Kirumba, Mwanza).
Oktoba 31 mwaka huu ni raundi ya tatu; Polisi Mara vs Rhino Rangers (Karume, Musoma), Morani vs Polisi Tabora (Kiteto, Manyara), Polisi Dodoma vs Pamba (Jamhuri, Dodoma) na Kanembwa FC vs
Mwadui (Lake Tanganyika, Kigoma).
MBAGA KUZICHEZESHA KENYA NA AFRIKA KUSINI
Mwamuzi Oden Mbaga wa Tanzania anayetambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) ndiye anayechezesha mechi ya kirafiki kati ya Kenya (Harambee Stars) na Afrika Kusini (Bafana
Bafana).
Mechi hiyo inachezwa leo Uwanja wa Kimataifa wa Moi Kasarani jijini Nairobi. Mbaga anasaidiwa na waamuzi wasaidizi wa FIFA, John Kanyenye kutoka Mbeya na Erasmo Jesse wa Morogoro.
TFF imeteua waamuzi hao baada ya kupata maombi kutoka kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) ambao ndiyo waandaaji wa mechi hiyo ambayo ni moja ya vipimo kwa kocha mpya wa Harambee Stars, Henry Michel kutoka Ufaransa.
TAFCA YAONGEZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU
Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) imeongeza muda kwa wagombea kuchukua fomu kwa ajili ya uchaguzi wa chama hicho ambao sasa utafanyika Novemba 25 mwaka huu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA, Ramadhan Mambosasa, jana ndiyo ilikuwa mwisho wa kuchukua fomu lakini mwitikio wa wagombea bado umekuwa mdogo ambapo ni watano tu waliojitokeza.
Hivyo, amesema wameongeza muda wa kuchukua na kurudisha fomu ambapo mwisho itakuwa ni Oktoba 19 mwaka huu saa 10 kamili alasiri. Fomu zinapatikana ofisi za TAFCA ambazo ziko Uwanja wa
Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Nafasi zinazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF, Mhazini na wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji.
MINTANGA AACHIWA HURU
Na Njumai Ngota
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, imemwachia huru aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa nchini (BFT), Alhaji Shaaban Mintanga, aliyeshtakiwa kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya.
Kuachiwa huru kwa Mintanga, kumetokana na mahakama kueleza kuwa, upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yake.
Jaji Dk. Fauz Twalib alitoa uamuzi huo jana, kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani, mbele yake ili kuamua endapo mshtakiwa huyo ana kesi ya kujibu au la.
Mintanga alikuwa akikabiliwa na mashtaka mawili ya kula njama na kusafirisha dawa za kulevya.
Kwa mujibu wa Jaji Twaib, upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi wanne, ambao ni Christopher Mutarukwa, Nassoro Irenge, Emilia Poliano na Charles Ulaya.
Alisema ushahidi wa Ulaya umezua hali ya kujikanganya katika kesi ya upande wa mashtaka, ikiwemo uzito wa dawa za kulevya, ambao kwenye hati ya kuonyesha thamani yake, inaelezwa ni kilo 4.8 na kwenye kielelezo cha nukushi kutoka Mauritius, inaonyesha ni kilo sita.
Jaji alisema ripoti kamili aliyopewa shahidi huyo hakuiwasilisha mahakamani kama kielelezo na hakuna shahidi yeyote aliyetoa ushahidi kuhusu idadi ya kilo za dawa hizo.
Alisema tangu awali, aliyekuwa akitafutwa kuhusika na usafirishaji wa dawa hizo ni mtuhumiwa Mika na si Mintanga na kwamba, mtuhumiwa Msengwa, ambaye anashikiliwa Mauritius, kwenye maelezo yake alisema hamfahamu Mintanga.
Ulaya katika ushahidi wake alidai kuwa, Msengwa alipatiwa dawa hizo na Mika katika hoteli iliyopo eneo la Manzese, Dar es Salaam na alikuwa akiwasiliana na mwanamke raia wa Kenya.
Jaji alisema upande wa mashtaka pia umeshindwa kuthibitisha mahali na tarehe, ambayo washtakiwa walikula njama.
Baada ya mahakama kumwachia huru Mintanga, ndugu, jamaa na marafiki waliokuwepo mahakamani walijawa na furaha kubwa na kumchukua ndugu yao na kutoweka naye.
Mintanga alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam, Julai 7, 2008 na hadi alipoachiwa huru, alikuwa amekaa rumande kwa zaidi ya miaka mitatu.
Monday, October 15, 2012
13 WAPITISHWA KUWANIA UONGOZI TWFA
Wagombea 13 kati ya 15 waliojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) wamepitishwa baada ya usaili uliofanyika juzi.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA, Ombeni Zavala, waliopitishwa kwenye nafasi ya uenyekiti ni Isabellah Huseein Kapera, Joan Ndaambuyo Minja na Lina Paul Kessy.
Makamu Mwenyekiti ni Rose Kisiwa wakati wanaowania nafasi ya Katibu Mkuu ni Amina Ali Karuma na Cecilia Oreste Makafu. Mgombea pekee wa nafasi ya Katibu Msaidizi, Macky Righton Mhango naye amepita kwenye usaili huo. Aliyepitishwa kwenye nafasi ya Mhazini ni Rose Stewart Msamila.
Furaha Francis na Zena Chande wamepitishwa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakati waliopita kuwania ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya TWFA ni Triphonia Ludovick Temba, Rahim Salum Maguza na Sophia James Charles.
Hivi mchakato wa uchaguzi wa TWFA uko katika kipindi cha kukata rufani ambapo ni kuanzia Oktoba 15-17 mwaka huu. Rufani zinatakiwa zifike kwa Katibu Mkuu wa TFF kabla ya saa 10 kamili jioni ya Oktoba 17 mwaka huu.
Wagombea wawili ambao hawakupitishwa kwa ajili ya uchaguzi huo
unaotarajiwa kufanyika Novemba 4 mwaka huu ni Julliet Mndeme na Jasmin Soud walioomba ujumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF. Wagombea hao ambao pia walikuwa wamewekewa pingamizi hawakufika kwenye usaili.
PONGEZI KWA UONGOZI MPYA ARFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Oktoba 14 mwaka huu).
Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa COREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Pwani.
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya COREFA chini ya uenyekiti wa Hassan Othman Hassan ambaye amechaguliwa tena kuongoza chama hicho.
Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu mkoani Pwani kwa kuzingatia katiba ya COREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya COREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za wanachama wa TFF.
Viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo ni Hassan Othman Hassan (Mwenyekiti), Riziki Majala (Katibu), Geofrey Irick Nyange (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF), Juma Haruna Kisoma (Mwakilishi wa Klabu TFF) na Abubakar Allawi (Mhazini).
Waliochaguliwa kuwa Wajumbe wa Kamati ya Utendaji katika uchaguzi huo uliofanyika kisiwani Mafia ni Musa Bakari Athumani, Godfrey Magnus Haule na Gwamaka Oden Mlagila. Mwakilishi wa Wanawake ni Florence Ambonisye.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Saturday, October 13, 2012
HATMA YA UCHAGUZI DRFA J'NNE
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekamilisha usikilizaji rufani zilizokatwa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA.
Ili kujiridhisha kuhusu uamuzi wote uliofanywa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA kuhusu waombaji uongozi wote wa DRFA waliopitishwa na ambao hawakupitishwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Kamati itatangaza uamuzi wake kuhusu mchakato mzima wa uchaguzi wa DRFA siku ya Jumanne, Oktoba 16, 2012.
Kutokana na hali hiyo, Uchaguzi wa DRFA uliokuwa ufanyike Oktoba 14, 2012 umeahirishwa hadi hapo uamuzi kuhusu uchaguzi huo utakapotangazwa Jumanne, Oktoba 16, 2012.
Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Katibu- Kamati ya Uchaguzi TFF
DEWJI ATOA SOMO KWA KLABU ZA LIGI KUU
WAKATI klabu za Yanga na African Lyon zikiendelea kusuguana namdhamini wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, kampuni ya simu ya mkononi yaVodacom, klabu za soka nchini zimeaswa kuanza kujitambua ili ziwezekunufaika kwa mambo mengi zaidi, badala ya kutumia muda mrefukulumbana kwa mambo madogo, akitolea mfano wa nembo ya Vodacom katikajezi za klabu.
Ushauri huo umetolewa na mfadhili wa zamani wa Simba, mfanyabiasharaAzim Dewji aliyesema kuwa, kama klabu za Tanzania
zingekuwazinajitambua, kamwe zisingepoteza muda kwa malumbano ya nembo, balimaslahi.
Akizungumza jana, alisema klabu kubwa kama Simba na Yanga, zinapaswakujenga hoja nzito kwa wadhamini, ili ziweze kunufaika zaidi kwa kuwazina thamani kubwa kutokana na ukongwe wake na utajiri wa wafuasi kotendani na nje ya Tanzania.
“Sawa wana haki, lakini klabu zetu ifike mahali zijitambue. Wavukehapo, mfano Simba na Yanga si zijenge hoja za kupata fedha zaidi kwawadhamini kwamba ili zivae jezi na nembo, zilipwe vizuri kulingana nahadhi halisi ya klabu hizi.
“Haiingii akilini kuona zimeshindwa kujenga ushawishi hata baada
yakuwekwa kundi moja na timu ambazo hazina wanachama wala ofisi, lakinikwa mujibu wa mkataba zote
zinalipwa sh milioni 7 kwa mwezi.
“Jamani, hivi Yanga yenye utitiri wa wanachama na wafuasi, utajiri
wamajengo mfano jingo lake lina thamani ya bilioni 2, inalipwaje sawa naAfrican Lyon ambayo haina wanachama wala ofisi?
“Si kama naidharau Lyon, la hasha, bali ndio uhalisia kwa sababu kamani kunufaika, Vodacom itanufaika zaidi kwa Yanga kutokana na wafuasiwake wengi kuliko Lyon, kwanini wasitumie mwanya huo kujenga hoja?”alihoji Dewji na kuongeza kuwa, hadhi ya klabu za Simba na Yanga angalau
kila moja iambulie sh milioni 250 kwa mwaka, na jezi za hadhiya juu kulingana na hadhi ya klabu
zenyewe.
Aidha, alisema udhamini mnono wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) niuthibitisho tosha kuwa thamani ya Simba na Yanga. TBL kupitia bia yaKilimanjaro, inazidhamini Simba na Yanga kila moja kwa wastani wa shbilioni 1.5 kwa mwaka, udhamini ukigusa mishahara ya wachezaji na benchi la ufundi, mabasi, vifaa vya michezo, gharama za mikutano yakila mwaka na kadhalika.
“Una sasa, TBL si wadhamini wakuu wa soka ya nchi hii, lakini klabuhizi zinanufaika, kama ukweli ndio huo kwa nini wasimbane mdhamini waligi ili
wanufaike zaidi na badala yake wanabaki na malumbano ya nembopekee? Ni wakati wa klabu zetu kubadilika kwa sababu kote ulimwenguni,soka ni biashara kubwa mno,” alisema.
Kauli ya Dewji imekuja huku klabu za Yanga na Lyon zikiwa katikamgogoro juu ya kutovaa jezi zenye nembo ya Vodacom, Yanga ikisemahaiko
tayari kuvaa jezi zenye nembo nyekundu ya mdhamini huku Lyonikitaka iruhusiwe kuvaa jezi za mdhamini wake binafsi, kampuninyingine ya simu za mkononi ya Zantel.
Kutokana na mvutano huo, klabu hizo zimejiingiza katika hatari yakuadhibiwa, kwani Shirikisho la Soka nchini (TFF) limetishia kuchukuahatua dhidi
Subscribe to:
Posts (Atom)











