KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 23, 2013

AZAM KUHAMIA ZANZIBAR



Na Salum Vuai, maelezo, Zanzibar
UONGOZI wa klabu ya Azam umesema upo katika mchakato wa kuunda timu nyingine ya soka itakayoshiriki katika michuano ya ligi kuu ya Zanzibar.

Katibu Mkuu wa Azam, Nassoro Idrisa alisema kwa njia ya simu juzi kuwa, uamuzi wao huo umelenga kuongeza ushindani katika ligi kuu ya Zanzibar.

Idrisa alisema pia kuwa, uamuzi wao huo umelenga kufanikisha jitihada za Kampuni ya SSB, inayomiliki Azam, kuwekeza katika soka ili kuongeza ajira kwa vijana.

Alisema walianza mchakato huo miezi sita iliyopita na iwapo sheria zitaruhusu, timu hiyo itaundwa mara moja.

Alipoulizwa timu hiyo mpya ya Azam itaanzia daraja lipi, Idrisa alisema lengo lao ni kushiriki moja kwa moja katika ligi kuu ya Zanzibar.

"Tunachoweza kufanya ni kununua mojawapo ya klabu zinazoshiriki ligi kuu ya Zanzibar, japokuwa inaweza kuwa kazi ngumu,"alisema Idrisa.

Hata hivyo, Idrisa alisema iwapo watashindwa kununua timu ya ligi kuu, watafanya hivyo kwa timu za madaraja ya chini, hasa daraja la pili.

Idrisa alisema mpango wao huo pia umelenga kujenga timu imara na itakayokuwa na miundombinu yote muhimu ili kuwavutia vijana wengi zaidi kucheza soka.

Alisema SSB ni kampuni kubwa, ambayo imeamua kujitangaza kibiashara kwa kutumia mchezo wa soka.

"Kwa kuwa tunao wigo mkubwa wa biashara Zanzibar, tunatarajia hatua hiyo itasaidia sana kuipa hadhi kampuni kama tulivyofanya kwa Tanzania Bara,"alisema.

No comments:

Post a Comment