Monday, August 6, 2012

MUETHIOPIA ASHINDA MBIO ZA MARATHONI ZA OLIMPIKI

Mwanariadha Tiki Galana wa Ethiopia leo ameibuka mshindi wa mbio za marathoni kwa wanawake katika michezo ya Olimpiki inayoendelea mjini London, Uingereza.

Tiki alishinda mbio hizo kwa kutumia saa 2:23:07, ikiwa ni rekodi ya Olimpiki, akifuatiwa na Priscah Jeptoo wa Kenya na Tatyana Petrova wa Russia.

No comments:

Post a Comment